Sunday , 28 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Membe awakaribisha ACT-Wazalendo waliokatwa CCM
Habari za Siasa

Membe awakaribisha ACT-Wazalendo waliokatwa CCM

Benard Membe, Mgombea Urais kwa tiketi ya ACT-Wazalendo
Spread the love

MGOMBEA urais wa Tanzania kupitia chama cha upinzani ACT-Wazalendo, Bernard Kamillius Membe, amewakaribisha ndani ya chama hicho wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) waliokatwa kuwania ubunge. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Membe aliyewahi kuwa waziri wa mambo ya nje wa Tanzania kati ya mwaka 2007 hadi 2015 enzi za utawala wa awamu ya nne wa Rais mstaafu Jakaya Mrisho Kikwete, ametoa ukaribisho huo jana Alhamisi tarehe 20 Agosti 2020.

Mwanadiplomasia huyo mashuhuri nchini aliyejiunga na ACT-Wazalendo tarehe 7 Julai 2020 baada ya kufukuzwa ndani ya chama alichokulia cha CCM amesema, waliokatwa ndani ya chama hicho kuwania kugombea ubunge wajiunge na ACT-Wazalendo.

Jana Alhamisi, CCM ilitangaza majina ya walioteuliwa kugombea ubunge katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Jumatano tarehe 28 Oktoba 2020 huku ikishuhudia zaidi ya wabunge 70 wakishindwa kutetea nafasi zao.

https://twitter.com/BenMembe/status/1296562904431558658

Membe akitumia ukurasa wake wa Twitter ameandika “uteuzi wa CCM uliofanywa leo (jana) umenifurahisha sana! Nawapongeza wote waliobahatika kuteuliwa, lakini kubwa zaidi nawapa pole wale wote waliokatwa kwa sababu ya kuwa karibu nami.”

           Soma zaidi:-

“Hiyo ni baraka siyo balaa. Karibuni mjiunge na ACT- Wazalendo haraka ili safari iendelee!” ameandika Membe ambaye ni Mshauri Mkuu wa ACT-Wazalendo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde aibana kampuni kutimiza masharti ya mkataba

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameitaka Kampuni ya Xin Tai...

Habari za Siasa

Sauti ya Watanzania waeleza sababu za kuiunga mkono Chadema

Spread the love  KIKUNDI kinachojipambanua katika kupigania rasilimali na uhuru wa nchi,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

error: Content is protected !!