Wednesday , 8 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbowe apata pigo jingine, ampoteza mama mkwe
Habari za SiasaTangulizi

Mbowe apata pigo jingine, ampoteza mama mkwe

Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema
Spread the love

 

FREEMAN Mbowe, kiongozi wa chama kikuu cha upinzani Tanzania cha Chadema ameendelea kuandamwa na majanga baada ya kumpoteza mama mkwe wake, Johara Mtei (79). Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Johara amefikwa n amauti leo Ijumaa tarehe 20 Agosti 2021 katika Hospitali ya Aga Khan jijini Dar es Salaam, alipokuwa amelazwa kwa matibabu.

Marehemu Johara ni mke wa Edwin Mtei, mwasisi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) ambaye pia amewahi kuwa Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Mtei alikuwa Gavana wa kwanza wa Benki Kuu kati ya Juni 1966 hadi Januari 1974 katika utawala wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Msiba huo umetokea ikiwa ni siku 28 zimepita tangu Mbowe alipompoteza baba yake mdogo, Manase Alphayo Mbowe.

Johari Mtei

Manase alifikwa na mauti tarehe 23 Julai 2021, katika Hospitali ya Machame mkoani Kilimanjaro, alikokuwa anapatiwa matibabu baada ya kusikia taarifa za mwanae huyo Mbowe kufunguliwa kesi ya ugaidi.

Mbowe amemuoa Dk. Lilian, ambaye ni binti wa Edwin Mtei na marehemu Johara.

Mashinda Mtei, mtoto wa Edwin Mtei amesema, ni kweli mama yao amefariki na kwa sasa wanaelekea mkoani Arusha kutoka Dar es Salaam kwa ajili ya maandalizi ya maziko.

Mbowe ambaye yuko mahabusu kwenye kuta nne za Gereza Kuu la Ukonga jijini Dar es Salaam kwa tuhuma za uhujumu uchumi na kupanga njama ya ugaidi kwa zaidi ya mwezi sasa.

Vifo hivyo vyote vimetokea yeye akiwa gerezani ambapo kifo cha Manase hakuhudhuria msiba sanjali na huu wa mama mkwe wake.

Huu ni msiba wa tatu kumkuta Mbowe ndani ya wiki chache, baada ya kaka yake, Charles Mbowe, kufariki dunia, tarehe 8 Julai 2021, na mwili wake kuzikwa nyumbani kwao Machame mkoani Kilimanjaro, tarehe 12 Julai 2021.

Edwin Mtei

Viongozi mbalimbali wametuma salamu za rambirambi kupitia kurasa zao za kijamii akiwemo Katibu Mkuu wa Chadema, John John Mnyika ameandika “nimepokea kwa masikitiko taarifa ya kifo cha Johari Mtei-Mke wa Mzee Edwin Mtei Mwenyekiti muasisi wa Chadema. Poleni sana familia na ukoo kwa msiba. Tumweke Mzee Mtei kwenye maombi katika kipindi kigumu ambayo yeye na familia wanapitia.”

Naye Kiongozi wa ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe ameandika “nimepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za kifo cha Mama Johara Mtei, Mke wa Mzee Edwin Mtei (muasisi wa
Chadema na mkwe wa kaka Freeman Mbowe, mwenyekiti wa Chadema.

Pole nyingi kwa Mzee Mtei, Dk. Lillian Mtei, Mashinda Mtei na watoto wote. Mola ampumzishe Mama mahala pema peponi.”

1 Comment

  • Pole sana mtanzania mwenzetu,

    Poleni pia wote mnaohusika. Mioyo yenu iwe na amani na utulivu kipindi hiki cha maombolezo.

    Rafiki yako,

    Aliko Musa.

    Mbobezi Kwenye Majengo

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Rais Samia ni Mzanzibari: Shida Iko Wapi?

Spread the loveTAIFA linakabiliwa na upungufu wa fikra sahihi. Upungufu huu unaonekana...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Mpina mwiba CCM, ahofia kuzibwa mdomo

Spread the loveWAKATI Chama cha Mapinduzi (CCM), kikijinasibu kuwa kinara wa demokrasia...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Mabeyo ametuepusha

Spread the loveNIMEGUSWA na uadilifu, utiifu na uaminifu wa Mkuu mstaafu wa...

Habari za SiasaTangulizi

CCM yaitaka TAKUKURU kuichunguza Chadema tuhuma alizoibua Lissu

Spread the loveCHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimeitaka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana...

error: Content is protected !!