Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Mawe, miamba ya barafu yasababisha kipande cha njia Mlima Kilimanjaro kufungwa
Habari Mchanganyiko

Mawe, miamba ya barafu yasababisha kipande cha njia Mlima Kilimanjaro kufungwa

Spread the love

Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) limefunga kipande cha njia cha ‘ARROW GLACIER” ambacho hutumika na baadhi ya wageni wanaopanda mlima Kilimanjaro kupitia njia ya Machame, Umbwe, Lemosho na Londorosi kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Mvua hizo kwa mwaka huu zimekuwa kubwa kuliko ilivyozoeleka na kusababisha maporomoko ya mawe, miamba ya barafu na utelezi na hivyo kuwa hatari kwa watumiaji wa njia hiyo.

Taarifa iliyotolewa leo Jumamosi na Afisa Uhifadhi Mwandamizi Kitengo cha Mawasiliano-TANAPA Catherine Mbena imesema ukaguzi uliofanywa na timu ya wataalam ya Hifadhi ya Taifa Kilimanjaro ikishirikiana na wataalamu wa taasisi ya NOLS (National Outdoor Leadership School) wenye uzoefu katika masuala ya usalama mlimani, umeonyesha kuwa hali imezidi kuwa mbaya.

Amesema maporomoko ya mawe, miamba ya barafu na utelezi yameongezeka na kwamba kwa sasa si salama kwa watumiaji.

“TANAPA inasitisha matumizi ya kipande hicho cha njia na badala yake itumike njia ya kawaida ya kutokea Baranco kuelekea Karanga na Barafu hadi kufika kileleni mpaka pale mvua zinazoendelea kunyesha zitakapokoma na kufanyika ukaguzi kujiridhisha kuwa njia hiyo ni salama kwa wapanda mlima na watoa huduma mlimani.

“Kipande cha “ARROW GLACIER” kinaanzia karibu na kituo cha Baranco katika eneo la “LAVA TOWER” na kinapita kwenye kasoko (crater) kuelekea kileleni ambapo wageni hupendelea kupita eneo hilo kwa ajili ya kuona mandhari nzuri ya mlima na pia ni rahisi kwa wageni kufika kileleni,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yang’ara maonesho OSHA

Spread the loveBenki ya NMB imebeba tuzo ya kampuni bora kwenye sekta...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari Mchanganyiko

Chongolo aonya viongozi vijiji kutouza NIDA kwa wageni

Spread the loveMKUU wa Mkoa wa Songwe, Daniel Chongolo amewaonya viongozi wa...

error: Content is protected !!