Wednesday , 8 May 2024
Home Kitengo Maisha Afya Manumba: Bilioni 4.7 zimebadili afya Kigoma DC
Afya

Manumba: Bilioni 4.7 zimebadili afya Kigoma DC

Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri hiyo, Rose Manumba
Spread the love

SERIKALI ya awamu ya sita chini ya Rais Samia Suluh Hassan imetoa zaidi ya Sh bilioni 4.7 katika kuboresha huduma za afya halmashauri ya wilaya ya Kigoma na kuwezesha wananchi kuanza kupata huduma maeneo ya karibu. Anaripoti Faki Sosi …(endelea).

Akizungumza leo tarehe 15 Desemba 2023, ofisini kwake Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri hiyo, Rose Manumba amemshukuru Rais Samia kwa kuonyesha upendo kwa wananchi wa Kigoma ambapo kwa miaka mitatu sekta hiyo ya afya imebadilika kwa ukubwa wake.

Aidha, amesema kuwa kiasi hicho cha fedha kimewezesha halmashauri hiyo kujenga vituo vitatu vya afya vipya, Hospitali ya wilaya sambamba na zahanati ambapo wananchi kwa sasa hawatembei umbali mrefu kuzifuata huduma hizo tofauti na ilivyokuwa miaka mitatu nyuma.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti wananchi katika halmashauri hiyo wameipongeza serikali kwa kuwaondolea adha ya kutembea umbali mrefu wa kufuata huduma za afya ambapo wameelezea kuwa kwa kipindi cha nyuma wanawake wengi walikuwa wakijifungulia njiani wakipelekwa kwenye zahanati za mbali na maeneo yao

James Kayunguye ni mganga mkuu wa halmashauri ya wilaya ya Kigoma ambaye amesema kuwa sekta ya afya katika halmashauri ya wilaya ya Kigoma imeimarika Zaidi kwa kuongezeka kwa vituo vya afya na zahanati hasa katika mwambao wa ziwa Tanganyika.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari MchanganyikoMakala & Uchambuzi

Kisukari cha mimba ni nini?

Spread the loveKisukari cha mimba ni aina ya kisukari kinachotokea kwa baadhi...

AfyaHabari Mchanganyiko

Huduma za kibingwa zazinduliwa katika hospitali za halmashauri 184

Spread the loveSERIKALI imezindua huduma za matibabu za kibingwa katika hospitali 184...

AfyaHabari Mchanganyiko

200 wapimwa afya na GGML katika maonesho ya OSHA

Spread the loveZAIDI ya watu 200 jijini Arusha wamejitokeza kupimwa afya na...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!