Sunday , 28 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mamia waupokea mwili wa Lowassa kimyakimya nyumbani kwake
Habari za Siasa

Mamia waupokea mwili wa Lowassa kimyakimya nyumbani kwake

Spread the love

 

HATIMAYE Mwili wa aliyekuwa Waziri Mkuu Mstaafu wa Tanzania, Hayati Edward Lowassa, umewasili nyumbani kwake Ngarash wilayani Monduli mkoani Arusha kutoka jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kutoa fursa kwa wakazi wa mji huo kutoa heshima za mwisho na kukamilisha taratibu za maziko. Anaripoti Mwandishi Wetu, Arusha … (endelea).

Msafara wa mwili huo uliowasili nyumbani hapa saa 8:50 mchana, ulipokewa kimyakimya bila vilio kutoka kwa mamia ya wakazi wa kijiji cha Ngarash, mkoa wa Arusha, viongozi na wageni mbalimbali.
Licha ya baadhi ya wananchi kutamani kugusa jeneza la mwili huo, hawakufua dafu kwani walinzi walihakikisha mwili huo umepelekwa katika nyumba maalumu iliyoandaliwa nyumbani kwake kwa maandalizi mengine.

Lowassa aliyefariki dunia tarehe 10 Februari mwaka huu, akipatiwa matibabu kwenye Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) , baada ya kuugua kwa muda mrefu, mwili wake unatarajiwa kuzikwa Jumamosi ijayo tarehe 17 Februari mwaka huu.

Mamia ya wakazi wa Arusha na Monduli walisimama pembeni ya barabara ambazo mwili wa Lowassa unapitishwa, kwa ajili ya kutoa heshima zao za mwisho.

Mwili wa Lowassa unatarajiwa kuagwa na wananchi kesho Ijumaa, kisha kuzikwa Jumamosi ambapo Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, anatarajiwa kushiriki mazishi hayo.

Enzi za uhai wake, Hayati Lowassa alifanikiwa kukonga nyoyo za watanzania wengi alipokuwa ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na hata alipohamia chama cha upinzani cha Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Sauti ya Watanzania waeleza sababu za kuiunga mkono Chadema

Spread the love  KIKUNDI kinachojipambanua katika kupigania rasilimali na uhuru wa nchi,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

error: Content is protected !!