MAKUSANYO ya Serikali katika mwaka wa fedha wa 2022/2023 yameongezeka kwa Sh. 3.582 trilioni, hadi kufikia Sh. 41.880 trilioni, kutoka Sh. 38.398 trilioni yaliyokusanywa 2021/2022. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).
Ongezeko hilo limebanishwa katika ripoti kuu ya ukaguzi wa Serikali kuu kwa 2022/2023, uliofanywa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Charles Kichere, ambayo imewasilishwa leo tarehe 15 Aprili 2024, bungeni jijini Dodoma.
Kwa mujibu wa ripoti hiyo, makusanyo yanayotokana na kodi, yasiyotokana na kodi na makusanyo ya halmashauri yaliyofadhili bajeti kwa Sh. 26.515 trilioni (63%), wakati yanayotokana na misaada na mikopo ni Sh. 15.365 trilioni (37%).
“Katika mwaka wa fedha wa 2022/23, Serikali ilikusanya Sh. trilioni 41.880, zaidi ya bajeti iliyoidhinishwa ya Sh. trilioni 41.480, ikiwa ni ongezeko la makusanyo kwa Sh. bilioni 400. Aidha, nilibaini ongezeko la makusanyo la Sh. trilioni 3.582, sawa na asilimia tisa ikilinganishwa na Sh. trilioni 38.298 zilizokusanywa katika mwaka wa fedha uliopita wa 2021/22,” imesema ripoti hiyo.
Leave a comment