Tuesday , 7 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Makamba ataja maeneo ya kuboresha mambo ya nje
Habari za Siasa

Makamba ataja maeneo ya kuboresha mambo ya nje

WAZIRI wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, January Makamba
Spread the love

 

WAZIRI wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, January Makamba ametumia takribani saa moja kuelezea maeneo ambayo yatajajadiliwa katika warsha ya Mabalozi wanaowakilisha Tanzania katika nchi mbalimbali duniani inayofanyika katika Chuo cha Uongozi cha Mwalimu Julius Nyerere mjini Kibaha kuanzia tarehe 21 hadi 24 Aprili 2024. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea). 

Makamba amewataka washiriki wa warsha hiyo ambao ni Makatibu Wakuu, Naibu Makatibu Wakuu, Mabalozi, Wakuu wa Utawala balozini, Wakurugenzi na Wakurugenzi Wasaidizi wa Wizara hiyo kujadili kwa upana maeneo hayo ili Wizara iweze kufikia malengo iliyowekewa na Serikali.

Maeneo ambayo ameyataja, Waziri Makamba ni pamoja na kuboresha mawasiliano ndani ya Wizara, baina ya Wizara na taasisi nyingine na wadau wake. Amesema hakuna namna Wizara ambayo majukumu yake ni uratibu ikafikia ufanisi unaohitajika bila kuwa na mfumo madhubuti wa mawasiliano.

Amesema eneo lingine ni umuhimu wa Wizara kuweka mfumo madhubuti zaidi wa kufuatilia utekelezaji wa matukio ambayo imekuwa ikiyaratibu tena kwa ufanisi mkubwa. Matukio hayo ni pamoja na masuala yanayoafikiwa katika ziara za viongozi, Mikutano, makongamano ambayo yana faida kubwa kwa nchi kama yatafuatiliwa vyema utekelezaji wake.

Aliongeza kuwa kuna umuhimu wa Wizara wa kuweka mfumo wa kuwaongezea maarifa, weledi na ujuzi maafisa wake, hususan katika uandishi na kuzungumza.

Amebainisha kuwa nchi yetu inasifika na kutangazika kutokana umahiri wa wanadiplomasia wake, jambo ambalo limekuwa ni kama urithi wetu, hivyo lazima jambo hili liendelezwe kwa kuwapatia watumishi ujuzi unaohitajika.

Pia amesisitiza ni umuhimu wa kuwa na mfumo wa kuwajibishana. Amesema mfumo huo utasaidia kuhamasisha utendaji kazi na kuongeza ufanisi katika Wizara.

Alisisitiza pia umuhimu wa kuendelea kulinda heshima na hadhi ya nchi yetu huko Nje. Alisema kuwa kufanikisha hilo ni pamoja na kuwa na mazingira bora ya utendaji kazi huko nje ikiwa ni pamoja na kuwa na vitendea kazi vinavyohitajika.

Alisema Serikali itahakikisha inaboresha mazingira ya kazi ili nchi iendelee kulinda heshima yake iliyojengwa kwa muda mrefu na viongozi waliopita.

Makamba alihitimisha mazurngumzo yake kwa kuwapongeza Mabalozi kwa kazi nzuri wanayofanya licha ya changamoto wanazokabiliana nazo. Amesema tokea ateuliwe kuwa Waziri wa Mambo ya Nje kwa muda wa miezi saba sasa amebaini kuna uwezekano wa kufanya mambo makubwa zaidi na ndiyo moja ya sababu ya kuitisha warsha hiyo ambayo ameitaja kuwa ni ya kubainisha changamoto, kuzitafutia ufumbuzi na kuweka mpango wa utekelezaji wenye tija kwa maslahi ya nchi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Jacob, Malisa wapandishwa kizimbani kwa mashtaka ya uongo mitandaoni

Spread the loveMKURUGENZI wa Shirika la Haki, Godlisten Malisa na mwanachama wa...

BiasharaHabari za Siasa

Bunge laitaka Serikali kudhibiti ufisadi miradi ya mkakati

Spread the loveKAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, imeitaka Serikali kuimarisha...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Wizara ya Uchukuzi yaomba kuongezewa bajeti na Bunge

Spread the loveWIZARA ya Uchukuzi imeliomba Bunge liidhinishe bajeti yake kwa mwaka...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali kutafuta mwekezaji mwingine Bandari ya Dar es Salaam

Spread the loveSERIKALI inaendelea kutafuta mwekezaji mwingine atakayeendesha gati namba nane hadi...

error: Content is protected !!