Sunday , 5 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Majaliwa: Wanaotorosha mbolea ya ruzuku Malawi ni wauaji…
Habari za Siasa

Majaliwa: Wanaotorosha mbolea ya ruzuku Malawi ni wauaji…

Spread the love

Waziri mkuu Kassim Majaliwa ameeleza kusikitishwa na kitendo cha baadhi ya watu wakiwemo mawakala feki wa mbole ‘vishoka’ wanaotorosha mbolea ya ruzuku kwenda nchini Malawi na kusisitiza kuwa watuhumiwa hao ni sawa na wauaji. Anaripoti Ibrahim Yassin, Songwe…(endelea).

Majaliwa ameyasema hayo leo tarehe 24 Novemba 2023 katika mkutano wa hadhara uliofanyika wilayani Ileje mkoani Songwe alipokuwa akizungumza na wananchi.

Amesema Serikali inawajali wakulima ndiyo maana imeletea mbole ya ruzuku ambayo kila mfuko mmoja wa mbolea una thamani ya Sh 50,000 ya Serikali.

“Mwaka jana walikamatwa watu kadhaa wakitorosha mbolea kwenda Malawi, adhabu kubwa itatolewa dhidi yao nawasihi wananchi acheni vitendo hivyo mtafungwa,” amesema Majaliwa.

Naye Mbunge wa Vwawa, Japhet Hasunga (CCM) amewapongeza wana-Ileje kwa kulima mazao mengi ya chakula na biashara lakini anashangaa kuona hawajui kutumia mazao hayo.

Amesema kitendo cha wananchi kulima mazao mengi alafu wanakuwa na kiwango kikubwa cha utapiamlo kinaitia aibu Ileje.

Naibu Waziri wa Ujenzi, Mhandisi Godfrey Kasekenya amesema kwa kushirikiana na uongozi wa halmashauri pamoja na mkuu wa wilayani watahakikisha wana wasimamia wananchi ili wapate mbolea.

Amesema kumekuwa na malalmiko kila kona kuhusu wakulima kutofikiwa na mbolea za ruzuku huku wakiendelea kuuzia mbolea kwa bei juu na mawakala vishoka.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Mbatia ambwaga Selasini, mahakama yaamuru alipwe fidia

Spread the loveMAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam, imemuamuru...

Habari za SiasaTangulizi

Mkulo afariki dunia, kuzikwa kesho Kilosa

Spread the loveALIYEKUWA Waziri wa Fedha na Mbunge wa Kilosa (CCM), Mustafa...

Habari za SiasaTangulizi

Sabaya afutiwa kesi, ruksa kugombea uongozi

Spread the loveMwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali DPP leo Ijumaa amefuta rufaa...

Habari za Siasa

Serikali yasaka bilioni 3 kujenga daraja Mto Mpiji

Spread the loveSerikali imesema inaendelea na juhudi za kutafuta fedha kiasi cha...

error: Content is protected !!