Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Majaliwa aahirisha Bunge, miswada minne na maazimio mawili yapitishwa
Habari za Siasa

Majaliwa aahirisha Bunge, miswada minne na maazimio mawili yapitishwa

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa
Spread the love

WAZIRI Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa, ameahirisha shughuli za Bunge hadi tarehe 1 Novemba 2022,zitakaporejea. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Majaliwa ameahirisha shughuli hizo leo Ijumaa, tarehe 23 Septemba 2022, bungeni jijini Dodoma, katika mkutano wa nane, kikao cha tisa cha Bunge.

Akielezea shughuli zilizofanyika katika mkutano huo wa nane wa Bunge, amesema maswali ya msingi 153 na ya nyongeza 467 ya wabunge, yaliulizwa na kujibiwa na Serikali.

Aidha, Majaliwa amesema katika mkutano huo miswada minne ya sheria ambayo ni Muswada wa Sheria ya Usimamizi wa Maafa wa 2022, Muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Usimamizi wa Rasilimali za Maji wa 2022, Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali za Fedha wa 2022 na Muswada wa Sheria za Marekebisho ya Sheria Mbalimbali Namba mbili wa 2022.

Waziri Majaliwa amesema, kupitia mkutano huo wabunge walipitisha maazimio mawili ya Bunge, ambayo ni Azimio la Bunge la Kuridhia Itifaki ya Mktaba wa Nchi Huru za Afrika wa Kuzuia na Kupambana na Ugaidi wa 2004 na Azimio la Bunge la Kuridhia Itifaki ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), ya kuongeza mamlaka ya Mahakama ya Afrika Mashariki.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!