MAHAKAMA ya Katiba nchini Uganda jana tarehe 10 Januari, 2023 imefuta sehemu ya sheria ya mawasiliano ambayo imekuwa ikitumika kuwashtaki wakosoaji wa serikali, waandishi habari na waandishi wa vitabu. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).
Sehemu ya sheria hiyo ya matumizi mabaya ya Kompyuta, ilikuwa inakataza matumizi ya mawasiliano ya kieletroniki kuvuruga amani, utulivu au haki ya faragha ya mtu yeyote asiye na kusudio la kufanya mawasiliano.
Adhabu ya wanaokiuka sheria hiyo ilikuwa ni faini ya fedha na kifungo cha hadi miaka saba gerezani.
Katika uamuzi wa kesi hiyo iliyofunguliwa na mwanaharakati mmoja nchini Uganda, Mahakama ya Katiba imekubali ombi hilo na kusema sehemu hiyo ya sheria inakiuka katiba.
Jaji wa Mahakama ya Katiba, Kenneth Kakuru amesema kifungu hicho cha sheria ni batili, kwani kinabinya uhuru wa kujieleza katika jamii huru na ya kidemokrasia.
Leave a comment