Friday , 26 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Mahakama Uganda yafuta sheria ya tata ya mawasiliano
Kimataifa

Mahakama Uganda yafuta sheria ya tata ya mawasiliano

Spread the love

 

MAHAKAMA ya Katiba nchini Uganda jana tarehe 10 Januari, 2023 imefuta sehemu ya sheria ya mawasiliano ambayo imekuwa ikitumika kuwashtaki wakosoaji wa serikali, waandishi habari na waandishi wa vitabu. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Sehemu ya sheria hiyo ya matumizi mabaya ya Kompyuta, ilikuwa inakataza matumizi ya mawasiliano ya kieletroniki kuvuruga amani, utulivu au haki ya faragha ya mtu yeyote asiye na kusudio la kufanya mawasiliano.

Adhabu ya wanaokiuka sheria hiyo ilikuwa ni faini ya fedha na kifungo cha hadi miaka saba gerezani.

Katika uamuzi wa kesi hiyo iliyofunguliwa na mwanaharakati mmoja nchini Uganda, Mahakama ya Katiba imekubali ombi hilo na kusema sehemu hiyo ya sheria inakiuka katiba.

Jaji wa Mahakama ya Katiba, Kenneth Kakuru amesema kifungu hicho cha sheria ni batili, kwani kinabinya uhuru wa kujieleza katika jamii huru na ya kidemokrasia.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!