RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan leo Jumamosi amefanya uteuzi na kuwahamisha vituo wakuu wa mikoa na kuwaacha kando watatu. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).
Walioachwa ni aliyekuwa mkuu wa mkoa wa Tanga, Waziri Kindamba ambaye nafasi yake imechukuliwa na wa Dk. Batilda Buriani aliyetokea Tabora. Hata hivyo, Kindamba ameteuliwa kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Mabasi Yaendayo Haraka (UDART) na kuchukua nafasi ya Gilliard Wilson Ngewe ambaye atapangiwa kazi.
Kanali Laban Thomas aliyekuwa mkuu wa mkoa wa Ruvuma naye panga limemkuta baada ya nafasi yake kuchukuliwa na Col. Ahmed Abbas Ahmed aliyehamishwa kutoka Mtwara.
Naye Dk. Fransis Michael aliyekuwa mkuu wa mkoa wa Songwe pia nafasi yake imechukuliwa na Daniel Chongolo aliyekuwa Katibu mkuu wa CCM aliyejiuzulu wadhifa huo mwaka jana.
Namfahamu vzr Dk Michael ni mchapa kazi mahiri, muwazi, mwenye uwezo Kama Katibu Mkuu na au Mtendaji mkuu wa taasisi yenye kuleta matokeo makubwa. Siasa hasha.
Nimefurahi sana kwa Daniel chongolo kurudi shwa! Daa huyu baba aliniuma sana moyo kwa kujiudhuru uongozi! Mungu mkubwa! Pongezi sana q kwako Mwanamke Jasiri,mwenye kuipambania Nchi yetu,usiyeyumba,Mama bora mwenye kuyaweka moyoni bila kukasirika juu ya Matusi ,kebehi za wapinga ubora wa majitoleo yako kwa Taifa letu ,Mama Samia Rais wangu Mungu akutetee na akutie nguvu🙏🙏🙏♥️♥️♥️