Thursday , 2 May 2024
Home Kitengo Michezo Lavaud agonga kolabo ya kibabe na Tiwa Savage…
Michezo

Lavaud agonga kolabo ya kibabe na Tiwa Savage…

Spread the love

STAA wa kike kwenye uwezo mkubwa katika kuimba na kutunga, Lavaud amerejea kwa kishindo baada ya kuachia singo kali inayokwenda kwa jina la “Roll on Me” – ikiwa kwenye mitandao ya Saint & Citizen Music. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Katika singo hiyo, amewashirikisha mastaa kadhaa wa muziki Afrika wakiwemo, Tiwa Savage,
Patoranking, Reekado Banks na Kanis.

Kwa hakika mastaa hao wamezidi kuinogesha singo hiyo na kuifanya yenye ladha ya kipekee.

Kwenye “Roll on Me” kuna mikono ya maprodyuza wakali, kama Kel-P, ambaye amepata kufanya kazi na wasanii Burna Boy, Wizkid, Rema na Trakmatik.

Akizungumzia traki hiyo, Lavaud anasema: “Nimefurahi sana kufanya kazi na wasanii wakubwa wenye uwezo na vipaji vya aina yake, lakini zaidi timu nzima ya utayarishaji. Nimependa jinsi tulivyoonyesha tamaduni na mila zetu za Kiafrika kwenye wimbo huo ambazo kwa hakika zimeongeza uzuri na upekee wa singo hiyo.”

Naye Tiwa Savage amesema: “Pale wasanii wanapokutana pamoja, kama hivi, kitu fulani cha kuvutia hutokea… na ndivyo ilivyokuwa.

“Huu wimbo ni mzuri na wa kipekee, nimefurahishwa na mchango wa kila mmoja wetu katika hii kazi.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

Michezo

Usiku wa Ulaya umerejea kibabe kabisa

Spread the love  LIGI ya Mabingwa barani Ulaya imerejea tena na awamu...

Habari MchanganyikoMichezo

Mambo ya Ndani, Ulinzi zang’ara michezo ya Mei Mosi Arusha

Spread the loveRais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini (TUCTA), Tumaini...

Michezo

Beti na Meridianbet mechi za leo

Spread the love IKIWA leo hii ni Jumapili tulivu kabisa, Meridianbet wanamkwambia...

error: Content is protected !!