JESHI la Uganda limedai kumuua mmoja wa makamanda wa kundi la waasi wa ADF lenye mafungamano na wanamgambo wa dola la Kiislamu nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa…(endelea).
Taarifa ya jeshi hilo iliyotolewa jana Ijumaa imesema, kamanda huyo aliyetambulika kwa jina moja la Fazul, alikuwa raia wa Tanzania na amekuwa akiendesha operesheni katika bonde la Mwalika kwenye mkoa wa Kivu.
Waasi wa ADF wamekuwa wakiendesha shughuli zao kwenye misitu Mashariki mwa Kongo kwa zaidi ya miongo miwili na wamekuwa wakifanya mashambulizi ndani ya nchi hiyo na wakati mwingine nchini Uganda.
Kundi hilo halikutoa taarifa yoyote ya haraka kuhusu kifo cha kamanda huyo. Kampala kwa kushirikiana na jeshi la Congo imekuwa ikipambana na makundi ya wabeba silaha kwa karibu miaka miwili sasa.
Leave a comment