Friday , 29 September 2023
Home Habari Mchanganyiko Kiongozi wa waasi ADF aliyeuawa adaiwa kua Mtanzania
Habari Mchanganyiko

Kiongozi wa waasi ADF aliyeuawa adaiwa kua Mtanzania

Spread the love

JESHI la Uganda limedai kumuua mmoja wa makamanda wa kundi la waasi wa ADF lenye mafungamano na wanamgambo wa dola la Kiislamu nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa…(endelea).

Taarifa ya jeshi hilo iliyotolewa jana Ijumaa imesema, kamanda huyo aliyetambulika kwa jina moja la Fazul, alikuwa raia wa Tanzania na amekuwa akiendesha operesheni katika bonde la Mwalika kwenye mkoa wa Kivu.

Waasi wa ADF wamekuwa wakiendesha shughuli zao kwenye misitu Mashariki mwa Kongo kwa zaidi ya miongo miwili na wamekuwa wakifanya mashambulizi ndani ya nchi hiyo na wakati mwingine nchini Uganda.

Kundi hilo halikutoa taarifa yoyote ya haraka kuhusu kifo cha kamanda huyo. Kampala kwa kushirikiana na jeshi la Congo imekuwa ikipambana na makundi ya wabeba silaha kwa karibu miaka miwili sasa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Askari Polisi wa wanawake watakiwa kuchangamkia fursa za elimu

Spread the love  KAMISHNA wa Polisi Utawala Menejimenti ya rasilimali watu, CP...

Habari Mchanganyiko

Vijana 400 waguswa na programu ya “Learning for Life” ya SBL

Spread the love  PROGRAMU ya “Learning for Life” imetimiza dhamira ya Serengeti...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Stamico yafungua fursa za kiuchumi kwa makundi maalumu

Spread the loveSHIRIKA la Madini la Taifa (STAMICO) limemwaga neema kwa watu...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Maabara ya bilioni 5 upimaji madini yazinduliwa Geita, inapima kwa mionzi

Spread the loveZaidi ya Sh bilioni tano zimewekezwa katika kampuni ya MSALABS...

error: Content is protected !!