Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kinana: Vyama vinampongeza Samia namna anavyoongoza nchi
Habari za Siasa

Kinana: Vyama vinampongeza Samia namna anavyoongoza nchi

Abdulrahman Kinana
Spread the love

MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Bara, Abdulrahman Kinana, amesema vyama vya siasa vinampongeza Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, kwa namna anavyoongoza nchi, pamoja na kuimarisha umoja wa kitaifa. Anaripoti Matilda Peter, Dar es Salaam…(endelea).

Kinana ametoa kauli hiyo leo tarehe 31 Agosti 2023, akizungumza katika hafla ya kufunga Tamasha la Kizimkazi, visiwani Zanzibar.

“Nataka niseme sisi wana CCM tunajivunia uongozi wako na nina hakika mimi binafsi nina mazungumzo mara kadhaa na vyama vingine, hata juzi tulikaa siku tatu na vyama vyote katika Baraza la Vyama vya Siasa, kila chama kiliposimama, kilipongeza kwa namna unavyoiongoza nchi, ulivyoleta maridhiano na ulivyoimarisha umoja wa taifa letu,” amesema Kinana.

Kuhusu tamasha hilo, Kinana amezitaka mamlaka zinazoandaa kuhakikisha wanaliboresha ili lipate umaarufu nje ya Tanzania kwa ajili ya kuvutia watalii.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Sauti ya Watanzania waeleza sababu za kuiunga mkono Chadema

Spread the love  KIKUNDI kinachojipambanua katika kupigania rasilimali na uhuru wa nchi,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

error: Content is protected !!