Tuesday , 26 September 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Kinana: Vyama vinampongeza Samia namna anavyoongoza nchi
Habari za Siasa

Kinana: Vyama vinampongeza Samia namna anavyoongoza nchi

Abdulrahman Kinana
Spread the love

MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Bara, Abdulrahman Kinana, amesema vyama vya siasa vinampongeza Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, kwa namna anavyoongoza nchi, pamoja na kuimarisha umoja wa kitaifa. Anaripoti Mwandishi Wetu, Zanzibar…(endelea).

Kinana ametoa kauli hiyo leo tarehe 31 Agosti 2023, akizungumza katika hafla ya kufunga Tamasha la Kizimkazi, visiwani Zanzibar.

“Nataka niseme sisi wana CCM tunajivunia uongozi wako na nina hakika mimi binafsi nina mazungumzo mara kadhaa na vyama vingine, hata juzi tulikaa siku tatu na vyama vyote katika Baraza la Vyama vya Siasa, kila chama kiliposimama, kilipongeza kwa namna unavyoiongoza nchi, ulivyoleta maridhiano na ulivyoimarisha umoja wa taifa letu,” amesema Kinana.

Kuhusu tamasha hilo, Kinana amezitaka mamlaka zinazoandaa kuhakikisha wanaliboresha ili lipate umaarufu nje ya Tanzania kwa ajili ya kuvutia watalii.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia avunja bodi ya REA

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amemteua Balozi Jacob Kingu, kuwa...

Habari za SiasaTangulizi

Chande aliyeng’olewa TANESCO kwenda TTCL apelekwa Posta

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amemteua aliyekuwa, Mkurugenzi Mkuu wa...

Habari za Siasa

Kamugisha aanika utekelezaji mpango kazi 2022/23

Spread the loveMWENYEKITI wa Ngome ya Vijana ya Chama Cha ACT-Wazalendo Mkoa...

Habari za Siasa

Vijana ACT-Wazalendo wakabidhiwa kivumbi kulinda kura uchaguzi 2024,2025

Spread the loveNGOME ya Vijana ya Chama cha  ACT-Wazalendo, imetakiwa kuwanoa wafuasi...

error: Content is protected !!