Friday , 26 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Kampuni za kigeni zahofia kuendelea na biashara China
Kimataifa

Kampuni za kigeni zahofia kuendelea na biashara China

Jiji la Beijing
Spread the love


OPERESHENI ya kiuchunguzi inayofanywa na Serikali ya China kwa kampuni za kigeni imeibua wasiwasi kwa kampuni hizo na kupelekea kufunga biashara zao nchini humo, Imeripoti New York Times … (endelea).

Kampuni hizo ni pamoja na Mintz Group, Bain Capvision Partners.

Kwa mujibu New York Times, China imekuwa ikilenga makampuni mashuhuri ya ushauri na uhusiano wa kigeni kwa kuyaweka viziuzini.

Inaelezwa kuwa kampuni hizo zinafanyakazi ya ushauri kwa wafanyabiashara wa kigeni nchini China kwa kufanya kutathmini uwekezaji kabla ya uwekezaji.

Mwezi Machi mwaka huu, Waziri wa Biashara wa China, Wang Wentao alitoa ahadi ya kuondosha vikwazo kwa kampuni hizo ili kampuni za kigeni ziwekeze zaidi.

Mbali na usumbufu wa sera ya sifuri ya Covid 19 Biashara za Kimataifa zinazovishwa na mzozo wa kisiasa wa kijiografia kati ya Washington na Beijing uliongeza hatari na kulazimisha mashirika mengi ya kimataifa kuandaa mipango ya dharura kwa njia mbadala ya China za kibiashara China.

Ulengaji wa hivi majuzi wa makampuni ya ushauri na uhusiano wa kigeni kupitia uvamizi, kuwekwa kizuizini na kukamatwa kumezua wasiwasi kuhusu kufanya biashara nchini China.

Xi Jinping, Rais wa China

Dan Harris Mwanasheria wa Seattle anayefanya kazi na kampuni za kigeni nchini humo, ameshauri kuwa ili biashara ya Beijing iendelee basi Rais Xi Jinping, kiongozi mkuu wa China, hana budi kuimarisha usalama kwa kampuni za kigeni.

Harris alisema kuwa idadi kubwa ya wafanyabiashara katika wiki za hivi karibuni wakitafuta njia za kupunguza uwepo wao nchini China.

Mmoja wa wateja wake, mtengenezaji wa samani wa Marekani, anashughulikia mpango wa kusambaza bidhaa zake kupitia kampuni ya kichina ili iweze kuwaondoa wafanyakazi wake wa kimarekani nchini humo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!