KAMATI Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa, ikiongozwa na Mwenyekiti wa CCM na Rais Samia Suluhu Hassan, imemteua wa Bahati Keneth Ndingo kuwa mgombea wa ubunge kwa tiketi ya CCM katika Jimbo la Mbarali, mkoani Mbeya. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).
Uchaguzi huo mdogo wa ubunge umepangwa kufanyika tarehe 19 Septemba 2023, kutokana na kifo cha aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo, Francis Leonard Mtega aliyefariki dunia tarehe 1 Julai 2023.
Kamati hiyo imekutana leo Alhamis katika kikao chake maalum, kilichofanyika Ikulu ya Chamwino, jijini Dodoma na kumteua Bahati ambaye sasa ni Mbunge wa Viti Maalumu CCM.
Aidha, Kamati Kuu ya CCM, imezipongeza Serikali zake zote mbili, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, inayoongozwa na Rais Samia na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, chini ya Dk. Hussen Ali Mwinyi, kwa namna zinavyoendelea kuwatumikia wananchi kwa vitendo kupitia utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya Mwaka 2020- 2025.
Leave a comment