Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Wakili: Mwabukusi mgonjwa, ana mshono
Habari za SiasaTangulizi

Wakili: Mwabukusi mgonjwa, ana mshono

Wakili Boniface Mwabukusi
Spread the love

WAKILI Philip Mwakilima ambaye anasimamia kesi inayomkabili ya Wakili Boniphace Mwabukusi na wenzie leo Alhamisi amesema mteja wake anaumwa hivyo Jeshi la Polisi limfikishe haraka mahakama pamoja na watuhumiwa wenzie ili wapate haki zao kisheria. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Wakili Mwakilima amesema mteja wake Mwabukusi ni mgonjwa, analala sakafuni huku akiwa na mishono mingi.

Bila kuutaja ugonjwa unaomsumbua Mwabukusi, Mwakilima ametoa wito kwa Rais Samia Suluhu Hassan kuingilia kati sakata hilo huku akitoa wito kwa jeshi la polisi kuwafikisha mahakamani watuhumiwa hao.

Wakili Mwabukusi aliyekuwa anasimamia kesi ya kupinga baadhi ya vifungu vya mkataba wa uwekezaji bandarini, Balozi Dk. Willibroad Slaa na Kada wa Chadema, Mpaluka Said Nyagali maarufu Mdude Nyagali  walikamatwa kwa nyakati tofauti wiki iliyopita kwa tuhuma za uchochezi na uhaini.

Hayo yalijiri baada ya Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP, Camillius Wambura kuutangazia umma kuwa kuna watu wamepanga maandamano yenye uchochezi na malengo ya kupindua serikali.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za SiasaTangulizi

Samia awataka watanzania kudumisha muungano

Spread the loveRais wa Tanzania,Samia Suluhu Hassan amewataka Watanzania kuendeleza Muungano kwa...

error: Content is protected !!