Friday , 2 June 2023
Home Kitengo Michezo Hatma ya Lulu kubaki uraiani au lupango, yamebaki masaa
MichezoTangulizi

Hatma ya Lulu kubaki uraiani au lupango, yamebaki masaa

Elizabeth Michael (Lulu) akitokea katika Mahakama Kuu
Spread the love

MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam kesho inatarajiwa kutoa hukumu ya kesi ya kuua bila kukusudi inayomkabili Msanii wa filamu Elizabeth Micheal, (Lulu), anaandika Faki Sosi.

Lulu anatuhumiwa kuwa Aprili 7, 2012 alimuua bila kukusudia msanii mwenzake Steven Kanumba bila ya kukusudia, Jaji Sam Rumanyika ndiye atakayetoa hukumu hiyo kesho.

Endapo Jaji atamkuta Lulu hana hatia atamuacha huru na akimkuta na hatia ya kuua bila kukusudia adhabu za makosa hayo hutofautiana kutokana na mazingira ya tukio jinsi lilivyotokea, ushahidi uliowasilishwa mahakamani na mwenendo wa kila siku wa mtuhumiwa.

Rekodi ya mtuhumiwa itazingatiwa kwenye hukumu hiyo kama alishawahi kufanya kosa kama hilo au makosa mengine kipindi cha nyuma pamoja na tabia zake kiujumla.

Upande wa Jamhuri ulileta mahakamani mashahidi wanne wakiwemo Seth Bosco ambaye ni mdogo wake Marehemu Kanumba, waliokuwa wakiishi kwenye nyumba moja na marehemu na alikuwepo siku ya tukio, Dk. Paplas Kagaiga aliyekuwa Daktari wa familia hiyo ambaye aliyefika nyumbani kwa Marehemu Kanumba mara baada ya kudondoka.

Wengine ni Daktari kutoka kwenye Hospitali ya Taifa Muhimbili aliyeufanyia uchunguzi mwili wa Marehemu Kanumba pamoja askari ASP Ester aliyefanya upelelezi kwenye tukio hilo pamoja na kumtia mbaroni Lulu.

Lulu aambaye anatetewa na wakili Peter Kibatala, waliwasilisha mashahidi wa wawili ambao ni Lulu mwenyewe aliyehadithia mazingira ya tukio na kueleza kuwa hakuhusika kwa namna yoyote kwenye kifo cha Marehemu Kanumba.

Mbivu na mbichi kwenye kesi hii tutajua kesho saa 3 asubuhi kwenye Mahakama Kuu, MwanaHALISI Online itakujuza kila kitakachotokea katika hukumu hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

Bosi NIC apandishwa kizimbani, akabiliwa na mashitaka 365

Spread the love  ALIYEKUWA Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Bima la Taifa...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar: Bakharesa hajavamia shamba letu

Spread the love  IKULU Visiwani Zanzibar, imeeleza kuwa eneo la kiwanda cha...

Habari za SiasaTangulizi

Zanzibar watangaza rasmi kuwa shamba la Razaba ni mali yao

Spread the love  SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), imetangaza rasmi kwamba shamba...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Mwinyi azindua Kamati ya Maridhiano Visiwani

Spread the love  RAIS wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Dk. Hussein...

error: Content is protected !!