Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Felix aongoza kwa 77%, Katumbi 15%
Habari za Siasa

Felix aongoza kwa 77%, Katumbi 15%

Spread the love

Wakati zoezi la kuhesabu kura likiendelea nchini Kongo, Rais Felix Tshisekedi ameendelea kuongoza kwa asilimia 77 na mpinzani wake wa karibu Moise Katumbi akifuatia kwa asilimia 15 katika jumla ya kura milioni tisa zilizohesabiwa hadi sasa.

Hayo yanajiri wakati upinzani ukiendelea kutoa madai ya udaganyifu katika uchaguzi huo na kutaka urudiwe. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa…(endelea).

Hadi usiku wa kuamkia jana Alhamis, Tume ya Uchaguzi nchini humo (CENI), ilitangaza matokeo ya kura zaidi ya milioni tisa ambazo tayari zimehisabiwa.

Rais Tshisekedi anayewania muhula wa pili ameonekana kupata kura zaidi ya milioni saba ambazo ni sawa na asilimia 77. Mpinzani wake wa karibu Moise Katumbi akiwa na asilimia 15 na Martin Fayulu akishika nafasi ya tatu na silimia 4 pekee.

Tshisekedi anaongoza kwa wingi wa kura katika majimbo 21 kati ya 26 ya Kongo pamoja na jiji kuu la Kinshasa huku Katumbi akiongoza katika majimbo manne ya kusini mashariki yakiwemo Haut-Katanga, Tanganyika, Lualaba na Haut-Lomami.

Matokeo ya mwisho ya uchaguzi wa Rais yanatarajiwa kutangazwa jumapili ya tarehe 31 Desemba 2023.

Upinzani umeyapinga matokeo hayo ya awali na kusema yalipangwa na Tume ya uchaguzi ili kumpa ushindi Rais Tshisekedi.

Olivier Kamitatu msemaji wa Moise Katumbi amesema uchaguzi lazima urudiwe na hivi karibuni watawasilisha malalamiko yao kwenye korti ya Katiba.

”Vyombo vyote vinavyosimamia mchakato wa uchaguzi vinaongozwa na wanachama wanaohusishwa na kabila la Félix Tshisekedi. Kwa hivyo, Mahakama ya Kikatiba inaendeleza tu udanganyifu ambao tayari umepangwa,” alisema Kamitatu.

Patrick Muyaya, msemaji wa serikali alikosoa vikali kauli hiyo ya msemaji wa Katumbi na kusema upinzani unapanga kuandaa vurugu.

Muyaya ameiambia DW kwamba machafuko hayatatokea na kuutaka upinzani kusubiri hadi matokeo kamili ya uchaguzi yatakapotolewa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari za Siasa

Wizara ya Kilimo yapanga kutumia Sh. 1.2 trilioni 2024/25

Spread the loveWIZARA ya Kilimo, imepanga kutumia bajeti ya Sh. 1.2 trilioni...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali yaanza msako wanaotoa mikopo kausha damu

Spread the loveSERIKALI imeanza kufuatilia watu, vikundi na taasisi zinazotoa kinyume cha...

error: Content is protected !!