Sunday , 28 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Familia ya Lowassa yafunguka, yamtaja Rais Samia
Habari za SiasaTangulizi

Familia ya Lowassa yafunguka, yamtaja Rais Samia

Spread the love

FAMILIA ya aliyekuwa Waziri Mkuu wa Tanzania, Hayati Edward Lowassa, imesema kiongozi huyo mstaafu alipigania uhai wake kabla ya mauti kumkuta. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Hayo yamesemwa leo Jumanne na Msemaji wa Familia ya Lowassa, Fredy Lowassa katika shughuli ya kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa mwanasiasa huyo aliyefariki dunia tarehe 10 Februari mwaka huu.

“Baba alipata umauti siku ya Jumamosi lakini kwa kweli tunasema tumelipokea hili kwa moyo wa imani kwasababu baba aligua muda mrefu, kama mlivyosema baba ni mpambanaji, kweli alipambana sana mpaka dakika ya mwisho lakini tunamshukuru Mungu na familia tumepokea kwa amani tunasema akapumzike kwa amani,” amesema Fredy.

“Kipekee naomba kutoa shukrani za familia kwa Rais Samia ukweli kama isingekuwa Rais Samia baba yetu asingefika hata hiyo Jumamosi. Mama Samia amekuwa ndugu, mlezi na mama mzazi kwetu kwa kweli hatuna cha kumlipa tunamshukuru sana. Siku anaondoka kuelekea Italia tayari hali ya baba ilikuwa imebadilika lakini alimtuma mkuu wa majeshi akawa anampa update kila baada ya nusu saa mpaka umauti unamkuta saa nane mchana,” amesema Fredy.

Amesema msiba huo sio wa ukoo wa Lowassa peke yake, bali wa taifa zima hasa wazazi na walezi ambao watoto wao wamesoma shule za sekondari za kata ambazo enzi za uhai wake akiwa Waziri Mkuu, Lowassa alisimamia ujenzi wake.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Biteko aipongeza GGML kudhibiti vifo, majeruhi mahali pa kazi

Spread the loveNAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari za Siasa

Askofu Shoo awataka ACT kupigania maslahi ya Taifa, wasikubali kuhongwa

Spread the loveALIYEKUWA Askofu Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri, Askofu...

Habari za Siasa

Biteko aagiza waajiri kudhibiti vifo mahali pa kazi

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde aibana kampuni kutimiza masharti ya mkataba

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameitaka Kampuni ya Xin Tai...

error: Content is protected !!