Tuesday , 14 May 2024
Home Habari Mchanganyiko DRC, Tz zasaini MoU Rais Tshisekedi akitua nchini
Habari MchanganyikoTangulizi

DRC, Tz zasaini MoU Rais Tshisekedi akitua nchini

Spread the love

Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan pamoja na Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) Felix Tshisekedi wameshuhudia utiaji saini hati ya makubaliano (MoU) baina ya nchi hizo mbili.

Utiaji saini wa hati hiyo inayohusu ushirikiano katika masuala ya teknolojia (ICT), posta na mawasiliano umefanyika leo tarehe 23 Oktoba, 2022 Ikulu jijini Dar es Salaam katika ziara siku mbili ya kikazi ya Rais Tshisekedi aliyetua nchini leo.

Mkataba huo unaohusu teknolojia umetiwa saini leo na Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Tanzania, Nape Nnauye pamoja na Naibu Waziri Mkuu wa Mambo ya Nje wa DRC, Christophe Lutundula.

Tanzania na DRC zimekubaliana kushirikiana na kuendeleza sekta ya mawasiliano kwa kuwa ni sekta pekee inayozalisha rasilimali pamoja na ajira kwa vijana kwa kiasi kikubwa.

Katika kukuza jitihada za biashara baina ya nchi hizo mbili, Rais Samia Serikali inafanya marekebisho ya meli ya Mv Sangara ili ianze tena kutoa huduma ya kusafirisha mizigo kati ya Tanzania na DRC.

Aidha, Rais Samia amesema Tanzania na DRC kupitia Jumuiya ya Afrika Mashariki zina mpango wa kujenga ushoroba wa kati wa barabara utakaounganisha nchi hizo mbili.

Takwimu za biashara baina ya nchi hizo mbili zimepungua kwa kipindi cha miaka 10 iliyopita hivyo nchi hizo mbili zimefufua Tume ya pamoja ya ushirikiano ili kukuza uhusiano na ushirikiano uliopo baina ya nchi hizo mbili.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaBiasharaHabari Mchanganyiko

EXIM Bank, Msalaba Mwekundu wapanda miti, wachangisha damu

Spread the love  BENKI ya Exim imeshirikiana na Chama cha Msalaba Mwekundu...

ElimuHabari Mchanganyiko

Waziri SMZ akoshwa na kazi za Global Education Link

Spread the loveSERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar SMZ imesema itaendesha msako na kuzifutia...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

CUF yajipanga kuelekea chaguzi zijazo

Spread the loveCHAMA cha Wananchi (CUF), kimejipanga kujijenga kisiasa kuelekea chaguzi zijazo...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yatoa vifaa tiba hospitali ya Mpitimbi Songea

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imetoa misaada ya vifaa...

error: Content is protected !!