Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa DPP amfutia kesi ya ugaidi kigogo wa ACT-Wazalendo
Habari za Siasa

DPP amfutia kesi ya ugaidi kigogo wa ACT-Wazalendo

Sylivester Mwakitalu, Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP)
Spread the love

 

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Tanga, imemuachia kwa masharti Mwenyekiti wa Chama cha ACT-Wazalendo, Ahmed Kidege na wenzake wawili, baada ya Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP), Sylvester Mwakitalu, kuiomba ifute kesi ya ugaidi iliyokuwa inawakabili mahakamani hapo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Masharti hayo ni, kuwa katika kipindi cha uangalizi wa muda wa miaka mitatu, ambapo Kidege na wenzake watakuwa wanaripoti Polisi kila Jumatatu ya mwanzo wa mwezi.

Taarifa hiyo imetolewa jana tarehe 25 Februari 2022 na Katibu Idara ya Haki za Binadamu na Makundi Maalum, ACT Wazalendo- Taifa, Mbarala Maharagande, muda mfupi baada ya Kidege na wenzake wawili, Ramadhani Songoro na Shaban Mohamed.

“Tarehe 25 Februari, 2022, Mahakama ya Hakimu Mkazi Tanga imefuta kesi ya ugaidi na uhujumu uchumi, iliyokuwa inamkabili dege na wenzake wawili. Hatua hiyo ya mnahakama imetokana na DPP kuwasilisha maombi ya kuifuta kesi hiyo,” imesema taarifa ya Maharagande.

Mbarara Maharagande, Katibu wa Idara ya Haki za Binadamu na Makundi Maalumu ya Chama cha ACT-Wazalendo

Kidege na wenzake walikaa rumande tangu tarehe 24 Septemba 2019.

Akizungumzia hatua hiyo, Katibu Mkuu wa ACT-Wazalendo, Ado Shaibu, amesema anaamini hayo masharti ya kuripoti Polisi, aliyopewa Kidege na wenzake, yataondolewa.

“Ni jambo la faraja kwa familia, chama na wapenzi wa haki nchini kuona Kidege na wenzake wameachiwa huru na kesi yao kufutwa baada ya kukaa gerezani kwa zaidi ya miaka miwili. Kwetu sisi, kila mwenzetu anaposhikwa na kufunguliwa kesi, kitu muhimu zaidi kwetu ni uhuru wake,” amesema Ado na kuongeza:

“Kwa namna yoyote ile. Ni matumaini yetu kuwa kupitia jitihada zetu, hata hayo masharti madogo ya kuripoti Polisi mara moja kwa Mwezi yataondolewa.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Spika Tulia aibana Serikali mafao ya wastaafu Jumuiya ya Afrika Mashariki

Spread the loveSPIKA wa Bunge, Dk. Tulia Ackson ameitaka Serikali kufanya tathimini...

Habari za Siasa

Serikali yawapa maagizo Ma-RC udhibiti magonjwa yasiyoambukiza

Spread the loveWAKUU wa mikoa nchini wametakiwa kuandaa utaratibu wa kuwawezesha wananchi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

error: Content is protected !!