Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Biden aimwagia Ukraine matrilioni kuendelea na vita
Kimataifa

Biden aimwagia Ukraine matrilioni kuendelea na vita

Spread the love

 

RAIS wa Marekani, Joe Biden ametia saini mkataba wa kutoa fedha kiasi cha Dola za Marekani milioni 600 (sawa na Sh trilioni 1.3) ikiwa ni msaada wa haraka wa kijeshi kwa taifa la Ukraine. Inaripoti Mitandao ya kimataifa … (endelea).

Agizo hilo linamuelekeza Waziri wa Mambo ya Nje ya Marekani, Antony Blinken kutoa msaada wa kijeshi wa haraka kwa Ukraine wa hadi dola za Marekani milioni 250 ili kulisaidia taifa hilo bila kuzingatia kifungu chochote cha sheria.

Awali zaidi ya dola za Marekani milioni 350 zaidi zilitengwa kwa ajili ya kutoa huduma za ulinzi na mafunzo ya kijeshi.

Biden alitoa pesa hizo jana tarehe 25 Februari, 2022 huku Rais wa Ukraine, Volodymr Zelensky akifichua kuwa alipuuza pendekezo la Marekani la kumtaka kuuhama mji mkuu wa Kyiv.

Rais wa Marekani, Joe Biden

Marekani ilimpa ofa hiyo Rais huyo wa Ukraine baada ya kupata taarifa kuwa Rais wa Urusi, Vladimir Putin ametuma vikosi vya utekaji nyara kumteka nyara au kumuua.

Zelensky alisema; Mapambano yapo hapa. Nahitaji risasi, si kupanda ndege na kukimbia.”

Kauli hiyo ya Zelensky imekuja saa chache kabla ya wanajeshi wa Urusi kudaiwa kuanza kuuzunguka mji wa Kyv wakati mapambano yakizidi kusika kasi kwa siku ya tatu sasa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!