Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Dk. Masumbuko Lamwai, afariki dunia
Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Dk. Masumbuko Lamwai, afariki dunia

Spread the love

DK. Masumbuko Mahunga Selasini Lamwai, aliyepata kuwa mbunge wa Ubungo (NCCR -Mageuzi) na mbunge wa kuteuliwa na Rais, mwanasheria nguli nchini, amefariki dunia. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Dk. Lamwai amefariki dunia majira ya saa sita za usiku wa jana Jumatatu, jijini Dar es Salaam.

Taarifa za kifo chake, zimetibitishwa na mdogo wake, Joseph Selasini. Joseph na Masumbuko, ni ndugu wa damu kwa baba na mama.

Selasini amesema, kaka yake huyo alizidiwa jana usiku na kupelekwa hospitali ya Rabininsia Memorial iliyopo Tegeta, jijini Dar es Salaam.

“Alipofika pale, wale madaktari wakawaambia huyu bwana ameshafariki. Inaonekana amekutwa na mauti, ama akiwa nyumbani au njiani wakati anapelekwa hospitali,” ameeleza Selasini ambaye ni mbunge wa Rombo, mkoani Kilimanjaro.

Katika kipindi cha uhai wake, Dk. Lamwai alikuwa mmoja wa vigogo wa upinzani nchini, ingawa baadaye mwaka 2000 alijiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Mwaka 1994, Dk. Lamwai alijitosa katika kinyang’anyiro cha uchaguzi wa udiwani katika kata ya Manzese, jimboni Ubungo. Akashinda na kuwa pekee wa upinzani wa kwanza mkoani Dar es Salaam.

Hakuishia hapo. Pamoja na kuwa diwani pekee wa upinzani, Dk. Lamwai aliamua kujitosa katika kinyang’anyiro cha kugombea umeya wa Jiji la Dar es Salaam, ambako aliambulia kura moja!

Akijibu swali la mmoja wa waandishi wa habari, kwamba kwa nini amegombea umeya huku akijua yupo peke yake na atashindwa?

Alijibu: “Nilitambua hilo, lakini sikutaka kupata dhambi kwa kumpigia kura mgombea wa CCM. Kumpigia kura mgombea wa CCM, kwangu ni dhambi kubwa.”

Baadaye Dk. Lamwai alisema, wale waliomnyima kura za kuwa Meya wao wa Jiji, wakipata wageni kutoka nje hna ambao hawafahamu Kiswahili, walikuwa wanamuita yeye kuwakilisha.

Katika uchaguzi mkuu wa mwaka 1995, Dk. Lamwai alijitosa kuwania ubunge katika jimbo la Ubungo. Akashinda na kuwa mbunge wa kwanza wa upinzani jijini Dar es Salaam, kupitia NCCR- Mageuzi.

Dk. Lamwai alijitosa katika kinyang’anyiro cha ubunge, wakati chama chake, kimewazuia wagombea wake kushiriki uchaguzi wa marudio, kufuatia kufutwa kwa uchaguzi wa kwanza katika mkoa mzima wa Dar es Salaam.

Dk. Lamwai atakumbukwa kama mwanasiasa machachari, mwanasheria nguli na mkufunzi mwandamizi (senior lecturer) wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Chuo Kikuu cha Tumaini.

Ndani ya NCCR-Mageuzi, alikuwa na wanasiasa wengine wakongwe kama vile Mabere Marando, Prince Bagenda, Anthony Komu, Dk. Sengondo Mvungi, Augustine Mrema, Dk. Ringo Tenga, Ndimara Tegambwage, Prof. Mwesiga Baregu, Dk. Haidar Maguto, James Mbatia, James Nyakyoma na wengineo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Serikali yaanza msako wanaotoa mikopo kausha damu

Spread the loveSERIKALI imeanza kufuatilia watu, vikundi na taasisi zinazotoa kinyume cha...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Equity Bank yaendelea kusotea mabilioni ya fedha mahakama rufani

Spread the loveBENKI za Equity ya Tanzania na Kenya, zimeendelea kupambana mahakamani...

Habari za Siasa

Spika Tulia aibana Serikali mafao ya wastaafu Jumuiya ya Afrika Mashariki

Spread the loveSPIKA wa Bunge, Dk. Tulia Ackson ameitaka Serikali kufanya tathimini...

Habari za Siasa

Serikali yawapa maagizo Ma-RC udhibiti magonjwa yasiyoambukiza

Spread the loveWAKUU wa mikoa nchini wametakiwa kuandaa utaratibu wa kuwawezesha wananchi...

error: Content is protected !!