RAIS Mstaafu, Dk. Jakaya Kikwete, amesema Lowassa alikuwa na mchango mkubwa kwa maendeleo ya nchi na ameacha alama. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).
Dk. Kikwete ametoa kauli hiyo akizungumza katika shughuli ya kumuaga Hayati Lowassa, leo Jumanne, jijini Dar es Salaam.
“Tumshukru Mungu Kwa muda aliotupatia kuishi na kuhudumiwa na Lowassa. wakati wa uhai wake ametoa mchango mkubwa kwa maendeleo ya nchi yetu na ameacha alama zitakazokumbukwa daima. Shukrani kubwa tunayoweza kutoa kwake kwa sasa ni kumuombea kwa mola aiweke roho yake mahala pema peponi,” amesema Dk. Kikwete.
Aidha, Dk. Kikwete ametoa pole kwa familia hususan mjane wa Hayati Lowassa, Regina Lowassa kwa kuondokewa na mpendwa wao.
Leave a comment