Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Dk. Festo Dugange arejea kazini
Habari za SiasaTangulizi

Dk. Festo Dugange arejea kazini

Spread the love

NAIBU Waziri Ofisi ya Rais – TAMISEMI, Dk. Festo Dugange leo Jumanne ameonekana kwa mara ya kwanza hadharani kwenye shughuli ya kiserikali ikiwa imepita miezi miwili na ushee tangu alipopata ajali tarehe 26 Aprili 2023. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Dk. Dugange awali aliripotiwa kulazwa katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Benjamin Mkapa Jijini Dodoma baada ya kupata ajali hiyo iliyozua maswali mengi na kuhusishwa na kifo cha mwanafunzi wa Chuo kikuu cha Dodoma (UDOM).

Ajali hiyo ilitokea katika barabara ya Iyumbu, maeneo ya St. Peter Clever ikihusisha gari namba T454 DWV aina ya Toyota Land Cruiser iliyokuwa ikiendeshwa na Dk. Dugange.

Hata hivyo, leo tarehe 25 Julai 2023 ameonekana akisalimiana na Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye (katikati) pamoja na Naibu Waziri wa Kilimo, Anthony Mavunde (kushoto) katika Maadhimisho ya siku ya Kumbukumbu ya Mashujaa katika Uwanja wa Mpya wa Mashujaa eneo la Mji wa Serikali – Mtumba, Dodoma.

Mgeni rasmi ni Dk. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!