NAIBU Katibu Mkuu Wizara ya Nishati nchini Tanzania, Kheri Abdul Mahimbali leo ametembelea Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam (DIT) na kupata fursa ya kuona ufungaji mfumo wa Gesi Asilia kwenye magari unaufanywa na wataalam wa DIT. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).
Mahimbila amesema lengo la ziara hiyo aliyoifanya jana Ijumaa tarehe 6 Mei 2022 ni kujifunza na kutangaza, kuelimisha na kuhamasisha Watanzania umuhimu wa kutumia gesi asilia.
Alitoa rai kwa DIT kutangaza na kuelimisha umma ili waione fursa hiyo na kuichangamkia.
“Serikali tunalisimamia jambo hili na tumeanza kuhamasisha magari ya serikali kuwekewa mfumo huu ili kupunguza matumizi ya dizeli na petroli,” alisema Mahimbila.
Hata hivyo, aliitaka DIT kujipanga kubadilisha mfumo wa dizeli pia kwa kuwa kwa sasa kazi kubwa inafanyika kwa magari ya petroli pekee.
Alisema magari ya mwendo kasi nayo yataingia katika mpango huo wa kutumia gesi siku za karibuni.
Katika ziara hii alitembelea karakana ya kuweka Mfumo wa Gesi kwenye magari (CNG) iliyopo DIT kuona uwekaji wa mfumo huo, ambapo kwasasa magari 149 ya Shirika la Maendeleo la Petroli (TPDC) unaendelea kwa makubalino yaliyoridhiwa na Kampuni Tanzu ya DIT (DIT Co. Ltd) na TPDC.
Leave a comment