Saturday , 27 April 2024
Home Kitengo Maisha Elimu DIT yatakiwa kujipanga kufunga mfumo wa gesi magari ya serikali, mwendokasi
Elimu

DIT yatakiwa kujipanga kufunga mfumo wa gesi magari ya serikali, mwendokasi

Spread the love

 

NAIBU Katibu Mkuu Wizara ya Nishati nchini Tanzania, Kheri Abdul Mahimbali leo ametembelea Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam (DIT) na kupata fursa ya kuona ufungaji mfumo wa Gesi Asilia kwenye magari unaufanywa na wataalam wa DIT. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Mahimbila amesema lengo la ziara hiyo aliyoifanya jana Ijumaa tarehe 6 Mei 2022 ni kujifunza na kutangaza, kuelimisha na kuhamasisha Watanzania umuhimu wa kutumia gesi asilia.

Alitoa rai kwa DIT kutangaza na kuelimisha umma ili waione fursa hiyo na kuichangamkia.

“Serikali tunalisimamia jambo hili na tumeanza kuhamasisha magari ya serikali kuwekewa mfumo huu ili kupunguza matumizi ya dizeli na petroli,” alisema Mahimbila.

Hata hivyo, aliitaka DIT kujipanga kubadilisha mfumo wa dizeli pia kwa kuwa kwa sasa kazi kubwa inafanyika kwa magari ya petroli pekee.

Alisema magari ya mwendo kasi nayo yataingia katika mpango huo wa kutumia gesi siku za karibuni.

Katika ziara hii alitembelea karakana ya kuweka Mfumo wa Gesi kwenye magari (CNG) iliyopo DIT kuona uwekaji wa mfumo huo, ambapo kwasasa magari 149 ya Shirika la Maendeleo la Petroli (TPDC) unaendelea kwa makubalino yaliyoridhiwa na Kampuni Tanzu ya DIT (DIT Co. Ltd) na TPDC.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

ElimuHabari za Siasa

MbungeCCM ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the love  MBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze...

ElimuHabari za Siasa

Walimu 52,551 kupandishwa madaraja mwaka huu

Spread the loveNaibu Waziri wa nchi, Ofisi ya Rais (Utumishi na Utawala...

BiasharaElimu

NMB yatoa vifaa vya ujenzi kwa shule sita Nyasa  

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa msaada wa vifaa mbalimbali vya ujenzi...

ElimuHabari Mchanganyiko

GGML yawapa mbinu wanafunzi Geita Boys kufikia malengo ya kitaaluma

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) imetoa mafunzo maalumu...

error: Content is protected !!