MKUU wa Wilaya ya Same mkoani Kilimanjaro, Edward Mpogolo amewataka wazazi wenye watoto wenye umri chini ya miaka mitano wawapeleke kupata chanjo ya polio awamu ya nne, inayotolewa wilayani humo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Kilimanjaro … (endelea).
Mpogolo amesema hayo jana tarehe 2 Disemba, 2022 baada ya kushiriki zoezi la utoaji chanjo hiyo katika Hospital ya Wilaya ya Same mkoani Kilimanjaro.
Amesema wazazi wanawajibu wa kuwapeleka watoto wao kupata chanjo hiyo, ili kuwakinga dhidi ya mlipuko wa ugonjwa wa kupooza (polio).
DC Mpogolo aliendelea kusisitiza kuwa Serikali imejipanga kukabiliana na magonjwa mbalimbali ikiwemo polio na kwamba watoa huduma ya afya na chanjo ya polio wanapita kutoa elimu kwa kila kaya juu ya mlipuko wa ugonjwa wa kupooza (polio) lengo ni kuwalinda watoto wote wawe salama maana ni taifa la kesho.
Kaimu Mganga Mkuu wa wilaya, Dk. Alex Alexander amesema timu ya wataalamu huduma ya chanjo ya polio imesambaa karibu vijiji vyote kutoa elmu juu ya mlipuko wa ugonjwa wa kupooza (polio) huku wakiakikisha mtoto chini ya umri wa miaka mitano anapata chanjo hiyo.
Mratibu wa Chanjo Wilaya ya Same, Happinus Pilula amesema hospital ya wilaya imejipanga kikamilifu kuhakikisha zoezi hilo la utoaji wa chanjo ya polio kwa watoto chini ya umri wa miaka mitano linakamilika na kuakikisha kila mtoto anapata chanjo hiyo.
Leave a comment