Friday , 3 May 2024
Home Habari Mchanganyiko COSTECH yawafungulia milango wabunifu
Habari Mchanganyiko

COSTECH yawafungulia milango wabunifu

Spread the love

TUME ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) imetoa fursa kwa wanafunzi wabunifu kujiunga na Kumbi mama ya bunifu Buni Hub ambayo inaendesha programu mbalimbali za ubunifu kwa lengo la kuendeleza na kukuza vipaji. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Akizungumza Jumapili tarehe 20 Machi 2022, na washiriki wa mashindano ya ubunifu   ya Teensinai Mkurugenzi wa Ubunifu na Teknolojia wa COSTECH, Dk. Gerald Kafuku amesema kuwa Tanzania imebeba hazina ya vipaji ambayo COSTECH inavigundua na kuvikuza na kwamba hazina hiyo inakwenda kuwa mlango wa mafanikio kwenye maendeleo ya Teknolojia nchini.

Mchuano huo ulidhaminiwa na Ubalozi wa Marekani nchini, na Smile Communication iliwashirikisha wabunifu wanafunzi waliotoka kwenye shule mbalimbali nchini.

Amesema COSTECH inakwenda sambamba na sera za maendeleo ya Taifa na kwamba Tume hiyo ina lengo la kuhakikisha wataalam wa Teknolojia hawatoki nje ya nchi.

Amefafanua kuwa COSTECH imeanzisha kumbi mama ya bunifu Buni Hub kwa lengo la kuwakuza wabunifu kama ambavyo tayari wabunifu wengine wamepaa kimataifa kupitia mpango huo.

“Hapa kwetu tumeanzisha mpango wa Buni kwa ajili ya vijana hawa wabunifu, na hapa tulishatengeneza vijana ambao ni mamilionea kwa sasa kutokana na COSTECH kuwapa mtaji, kuwaendeleza na kuwashika mikono.

“Tunawakaribisha wabunifu wote kuanzia sasa wajiandikishe hapa Buni ili tuwasaidie kwenye ubunifu wao wa kiteknolojia.

Rose Mariki mmoja wa majaji wa mashindano hayo ameipongeza COSTECH kwa kuendeleza vipaji vya ubunifu ambavyo Taifa litapiga hatua kwenye ubunifu huo.

Suleiman Abdallah Mshiriki wa mashindano hayo amesema kuwa shindano hilo limempa ujasiri na matumaini ya kukuza kipaji chake.

Nimefurahi kusikia COSTECH wametufungulia mlango wa fursa ya kutukuza nami najiona mbali kwenye ulimwengu wa Teknolojia.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

Kimbunga “HIDAYA” chaendelea kuimarika, wananchi wapewa tahadhari

Spread the loveMAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inaendelea kutoa taarifa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yang’ara maonesho OSHA

Spread the loveBenki ya NMB imebeba tuzo ya kampuni bora kwenye sekta...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

error: Content is protected !!