Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Chadema yaeleza sababu za kutekwa diwani wake
Habari za SiasaTangulizi

Chadema yaeleza sababu za kutekwa diwani wake

Spread the love

CHAMA cha Chadema kimehusisha tukio kutekwa kwa mgombea wa udiwani wa kata ya Buhangazi wilayani Muleba Mkoani Kagera, Nelson Makoti kuwa ni njama za kisiasa. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Katibu Mkuu wa Chama hicho, Vincent Mashinji ameeleza kuwa kutekwa kwa diwani huyo ni njama za siasa kutokana na viashiria vya kulazimishwa mgombea huyo kuwa ajiengue kwenye kinyang’anyoro hicho na kwamba atapewa shilingi milioni nane.

Mashinji ameleeza kuwa kiashiria kingine ni kulazimishwa ni kupigiwa simu kwa ndugu zake na mtu aliyetambuliwa kama John Rutenga ambao walishawishi kusihi kutoendelea na uchuguzi huo.

Amesema kuwa mgombe huyo alitekwa alipokuwa akitoka Bukoba Mjini alipokwenda kwa ajili ya kununua vifaa vya kampeni ambapo aliingizwa kwenye gari na kufungwa kitambaa cheusi.

Mashinji ameeleza kwa mujibu wa muhanga wa tukio hilo kuwa aliteswa na kulazimishwa kuacha kugombea nafasi hiyo.

Amesema ndugu na wanachama wa Chadema walikwenda kutoa taarifa kwenye kituo cha Polisi cha Buhangaza ambapo askari wa kituo hicho walisema kuwa tukio hilo ni kubwa hivyo waende kituo cha wilaya ya muleba ambako na huko walinyimwa (RB).

Mashinji ameshangazwa na kitendo cha jeshi la polisi kuwakamata viongozi wa chama hicho ilhali gari iliyofanya tukio hilo ipo na mmliki wake anajulikana.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Sauti ya Watanzania waeleza sababu za kuiunga mkono Chadema

Spread the love  KIKUNDI kinachojipambanua katika kupigania rasilimali na uhuru wa nchi,...

Habari MchanganyikoTangulizi

Jacob, Malisa waachiwa kwa masharti

Spread the love  JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

error: Content is protected !!