KATIBU wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Sophia Mjema, amesema hakuna chama cha siasa cha upinzani kitakachosumbua chama chake kwenye Uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa 2024. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).
Mjema ametoa kauli hiyo leo tarehe 15 Februari 2023, kupitia ukurasa wake wa Instergram, akizungumzia ziara yake ya kikazi ya siku mbili, aliyofanya mkoani Shinyanga.
Mwenezi huyo wa CCM amesema kuwa, chama chake kitachaguliwa na wananchi kutokana na weledi wa kazi inazofanya kupitia Serikali yake inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan.
“Jana tarehe 14 Februari 2023, nimewasili mkoani Shinyanga nikiwa katika ziara ya kikazi ya siku mbili. Nikizungumza na viongozi mbalimbali wa Chama cha Mapinduzi ngazi ya mkoa na Wilaya nimesisitiza kuwa hakuna chama chochote kitakachoisumbua CCM katika uchaguzi wa serikali za mitaa na uchaguzi mkuu,” ameandika Mjema na kuongeza:
“Viongozi wa Chama Cha Mapinduzi wana wajibu wa kujibu hoja mbalimbali kwa vitendo na ushahidi kamili kwani kufanya hivyo itaondoa majungu. Nimesisitiza kuwa viongozi hao wana wajibu wa kufanya kazi ya kutangaza sera za CCM na Ilani yake hivyo kupitia mikutano mbalimbali ya kuimarisha chama wanapaswa kueleza mafanikio ya serikali.”
Kama UMEPEWA PROJECT KITAMKWACHO HAYA TUTAONANA TENA YAWEE… TUTAONANA TENA.. TUTAONANA YAWE… TUTAONANA TENA… BIBI YAKO MPYA YAWEZEKANA ALIFIKA HUKU.. Je UNATAFUTA MWANAMKE NA HAUJAOA!? NUNUA PINDA HONEY… HUYU HAPA YUPO AVAILABLE..
https://www.picuki.com/media/2040637081931345491