CHAMA cha Mapinduzi (CCM) kimeendelea kuvigaragaza vyama vya upinzani baada ya kutetea jimbo la Mbarali katika uchaguzi mdogo uliofanyika jana Jumanne. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endeela)
Msimamizi wa uchaguzi jimbo hilo lililopo Mbeya, Missana Kwangura leo Jumatano amemtangaza Bahati Ndingo (CCM), kuwa mshindi katika uchaguzi mdogo wa jimbo hilo.
Ndingo amepata kura 44, 334 dhidi ya mshindani wake wa karibu, Modestus Kilufi wa ACT – Wazalendo, aliyepata kura 10, 014.
Uchaguzi huo umefanyika baada ya aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo, Francis Mtega kufariki dunia katika ajali ya pikipiki tarehe 1 Julai mwaka huu.
Leave a comment