Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa CCM yakemea ufisadi, yaipa kibarua TAKUKURU
Habari za Siasa

CCM yakemea ufisadi, yaipa kibarua TAKUKURU

Katibu Mkuu wa CCM, Dk. Emanuel Nchimbi
Spread the love

 

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimekemea vitendo vya ubadhirifu wa fedha za miradi inayoendelea kujengwa nchini, huku ikiiagiza Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini (TAKUKURU), kuifuatilia kwa karibu ili kudhibiti uchotwaji wa fedha za umma. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika jana tarehe 18 Aprili 2024, mkoani Njombe, Katibu Mkuu wa CCM, Dk. Emanuel Nchimbi, alisema wanaoliibia taifa ni sawa wanajiibia wenyewe na kukwamisha maendeleo ya taifa lao.

Dk. Nchimbi amewataka viongozi wa serikali kuwa na matumizi sahihi ya fedha za umma.

“Vyombo vyote vya Serikali vyenye mamlaka ya matumizi ya fedha za miradi, hakikisheni pesa hizo zinatumika kihalali na msisubiri kukamata walioiba bali ni lazima mdhibiti na kuzuia mianya ya uibaji,” alisema Dk. Nchimbi na kuongeza:

“TAKUKURU hakikisheni miradi yote hasa mikubwa ya maendeleo mnaifuatilia tangu ikiwa inaanza kuhakikisha hakuna fedha ya umma inaibiwa na kutumika vibaya, tunataka thamani ya fedha ieandane na thamani ya mradi husika. “

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Serikali yaanza msako wanaotoa mikopo kausha damu

Spread the loveSERIKALI imeanza kufuatilia watu, vikundi na taasisi zinazotoa kinyume cha...

Habari za Siasa

Spika Tulia aibana Serikali mafao ya wastaafu Jumuiya ya Afrika Mashariki

Spread the loveSPIKA wa Bunge, Dk. Tulia Ackson ameitaka Serikali kufanya tathimini...

Habari za Siasa

Serikali yawapa maagizo Ma-RC udhibiti magonjwa yasiyoambukiza

Spread the loveWAKUU wa mikoa nchini wametakiwa kuandaa utaratibu wa kuwawezesha wananchi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

error: Content is protected !!