Tuesday , 30 April 2024
Home Gazeti Habari Bunge lataka sekta ya mawasiliano iimarishwe
Habari

Bunge lataka sekta ya mawasiliano iimarishwe

Spread the love

 

KAMATI ta Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, imeishauri Serikali kuimarisha sekta ya habari na mawasiliano, kwa kuwa ni chachu ya maendeleo ya uchumi wa nchi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma…(endelea).

Wito huo umetolewa leo Ijumaa, tarehe 20 Mei 2022 na Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, Anne Kilango Malecela, akiwasilisha maoni na ushauri wa kamati hiyo kuhusu makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya HJabari kwa mwaka 2022/23.

Malecela amesema, kamati hiyo inaishauri Serikali itoe fedha za kutosha kufanikisha mradi wa Anwani za Makazi na Postikodi.

Mbali na wito huo, kamati hiyo imeishauri Serikali isimamie Shirika la Posta (TPC), lipate mikopo ili liweze kulipa madeni inayodaiwa kiasi cha Sh. 26.8 bilioni. Pia, imeshauri taasisi za Serikali zinazodaiwa na shirika hilo, zilipe madeni ili liweze kujiendesha.

Katika hatua nyingine, Malecela amesema kamati hiyo inaishauri Serikali kuliwezesha Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) na Kampuni ya Magazeti ya Serikali (TSN), ili zijiendeshe kibiashara kwa kuansiha miradi ya maendeleo.

“Serikali ihakikishe taasisi zake zinalipa madeni ya mashirika haya mfano, deni la TSN limefikia Sh. bilioni 11,” amesema Malecela.

https://www.youtube.com/watch?v=ZWV-O136fo0

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

HabariSiasa

Dk. Rose Rwakatare atoa kadi 500 kila Wilaya Morogoro

Spread the loveMWENYEKITI wa Jumuiya ya Wazazi CCM Mkoa wa Morogoro, Dk...

ElimuHabari

CBE, WMA wasaini makubaliano wanafunzi kusoma wakifanyakazi

Spread the loveNAIBU Spika Musa Azzan Zungu amekipongeza Chuo cha Elimu ya...

HabariTangulizi

Dk. Slaa, Mwabukusi kuhojiwa na jeshi la Polisi Mbeya

Spread the loveJESHI la Polisi jijini Mbeya, linawashikilia kwa mahojiano Dk. Wilbroad...

HabariHabari Mchanganyiko

Kairuki Hospital Green IVF  yawanoa madaktari kuhusu upandikizaji mimba

Spread the love KITUO cha Upandikizaji Mimba cha Kairuki Hospital Green IVF...

error: Content is protected !!