UONGOZI wa Mkoa wa Dar es Salaam, unaendelea na vikao vya kuandaa mpango wa wafanyabiashara kutekeleza shughuli zao usiku na mchana (saa 24). Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).
Kauli hiyo imetolewa leo Jumatatu na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, akizungumza na waandishi wa habari, jijini humo.
Chalamila amesema timu za wataalamu kutoka mamlaka mbalimbali ikiwemo vyombo vya ulinzi na usalama na wafanyabiashara zinaendelea kufanya mazungumzo ili kuangalia namna ya kutekeleza mpango huo bila kuleta madhara, huku akiweka wazi kwamba kuna baadhi ya sheria ndogo zitapaswa kurekebishwa ili kutokuwa kikwazo.
“Dar es Salaam ni mji mkubwa, wakati huu tunapoajiandaa kuanza biashara saa 24 kwa kukamilisha soko la Kariakoo, timu zetu zipo kwenye mazungumzo katika vikao vya awali. Taasisi za fedha, vyombo vya ulinzi na usalama na wafanyabiashara na mamlaka nyingine zote tunakamilisha model yetu itakayosaidia kuanzisha biashara kwa muda wa saa 24,” amesema Chalamila.
Leave a comment