Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Bei za petroli, dizeli yashuka Dar, mafuta ya taa yapaa
Habari MchanganyikoTangulizi

Bei za petroli, dizeli yashuka Dar, mafuta ya taa yapaa

Spread the love

MAMLAKA ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (Ewura) imetangaza bei mpya za nishati ya mafuta nchini ambazo zimeanza kutumika leo Novemba 1, 2023 huku katika mikoa ya Dar es Salaam, Tanga na Mtwara, mafuta ya petrol na dizeli zikionekana kushuka ilihali mafuta ya taa yakipanda. Anaripoti Mwandishi Wetu… (endelea).

Kwa mujibu wa tangazo hilo la Ewura katika mkoa wa Dar es Salaam, lita mmoja ya Petroli kwa bei ya rejareja itauzwa Sh 3,274, dizeli ni Sh 3,374 na mafuta ya taa yatauzwa kwa Sh 3,423.

Kutokana na tangazo hilo la bei hizo mpya, inaonyeshakuwa petrol imeshuka kwa Sh7 kwa lita wakati dizeli imeshuka kwa Sh74 kwa lita, huku mafuta ya taa yakipanda kwa Sh480 kwa lita, tofauti na bei kikomo zilizotangazwa mwezi uliopita kwa mkoa wa Dar es Salaam.

Katika mkoa wa Tanga, petroli itauzwa kwa Sh3,274 kutoka Sh3,327, huku dizeli ikiwa imepanda kutoka Sh3,494 hadi Sh3,510; na mafuta ya taa yatauzwa Sh3,469 tofauti na ilivyokuwa mwezi uliopita ambapo yaliuzwa Sh2,989.

Kwa upande wa mkoa Mtwara, petroli itauzwa Sh3, 347, dizeli  Sh3,546, mafuta ya taa yamepanda kutoka Sh3,016 had Sh3,495.

Ewura imesema mabadiliko ya bei za mafuta kwa mwezi Oktoba 2023 yanatokana na kupungua kwa bei za mafuta katika soko la dunia kwa wastani wa asilimia 5.68 na gharama za uagizaji wa mafuta kwa wastani wa asilimia 13 kwa petroli, asilimia 25 kwa dizeli na uamuzi wa wazalishaji wakubwa wa mafuta duniani (OPEC+) kupunguza uzalishaji na vikwazo vya kiuchumi ambavyo nchi ya Urusi imewekewa.

Aidha, imesisitiza wafanyabiashara wa bidhaa za mafuta kwa rejareja wanatakiwa kuuza mafuta kwa bei zilizotangazwa na mamlaka hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

Jacob, Malisa waachiwa kwa masharti

Spread the love  JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari Mchanganyiko

Polisi wakanusha kufanya uzembe ajali iliyouwa mwandishi Ayo Tv

Spread the loveJESHI la Polisi limekanusha tuhuma zilizoibuliwa dhidi yake  kwamba limekawia...

Habari Mchanganyiko

Rais Samia kuzindua gazeti litakalotoa habari za wafanyakazi Tanzania

Spread the loveSHIRIKISHO la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), liko mbioni kufufua...

error: Content is protected !!