Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL) imetoa ufatanuzi kuhusu mabadilko ya ratiba zake za safari za China kwa abiria wake kuwa zimetokana na ndege zote mbili za masafa marefu Boeing 787-7 (Dreamliner) kufikia muda wake wa matengenezo ya kawaida (maintenance schedule). Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Mawasllano kwa Umma kutoka ATCL, Sarah Reuben, matengenezo hayo yalipangwa kufanyika kwa awamu.
Hata hivyo, kutokana na kuvurugika kwa mfumo wa ugavi (supply chain) katika utengenezaji wa vipuri vya ndege uliosababishwa na athari za UVIKO 19; ratiba ya matengenezo ya kawaida kwa ndege hizo zote za Boeing 787-8 (Dreamliner), imepangwa kufanyika kwa pamoja ili kuondoa hatari ya kukosekana kwake kwa muda mrefu ikiwa watapoteza nafasi ya matengenezo waliyopangiwa.
“Huu ni utaratbu wa kawaida kwa Mashirka yote ya ndego duniani. Kama livyo kawaida, utaratibu maalum umeandalwa kwa abiria wote wa safari za Guangzhou, China ill safari zao ziendelea kama kawaida kama walivyofahamishwa hapo awali hadi ndege zitakaporejea,” imesema taarifa hiyo na kuongeza;
“ATCL Itaendelea kuhakikisha inatoa huduma bora kwa wateja huku kizingatia usalama wa abiria wake ikiwemo kuhakikisha matengenezo yanafanyka kama livyopangwa.”
Leave a comment