Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Akamatwa na stika 2,546 za Viza
Habari Mchanganyiko

Akamatwa na stika 2,546 za Viza

Spread the love

IDARA ya Uhamiaji nchini, imemkamata Jasmin Ngongolo, mkazi wa Dar es Salaam akiwa na stika za Viza 2,546 za Tanzania za kughushi. Anaripoti Hamis Mguta … (endelea).

Mwanamke huyo alikamatwa tarehe 02 Agosti 2019 saa saba usiku katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere, jijini Dar es Salaam (JNI) akitokea Afrika Kusini.

Samwel Mahirane, Kamishna wa Uhamiaji Usimamizi na Udhibiti wa Mipaka amesema, mtuhumiwa huyo alifunga mizigo hiyo kwa ustadi ikiwa na utambulisho juu ya kila boksi kuwa ni stika zinazobandikwa katika vioo vya magari.

Amesema, mtuhumiwa alikutwa na bidhaa nyingine ambazo ni sabuni za kuogea, sabuni za unga za kufulia, pampers, herein, pafyumu na vipodozi vya aina mbalimbali kwa lengo la kuwahadaa maofisa wakati wa upekuzi.

“Tumefanikiwa kumkamata pia na mume wa mtuhumiwa ambaye ni Zakayo Stanslaus na anahusishwa na hujuma hiyo kwa kufika uwanja wa ndege kwa ajili ya  kumpokea mtuhumiwa,” amesema.

Inaelezwa, kukamatwa kwa watuhumiwa hao kunafuatia taarifa kutoka kwa wasamaria wema na kwamba, baada ya kukamilika kwa uchunguzi, watuhumiwa hao na watakaohusishwa na mtandao huo, watafikishwa mahakamani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NEMC yatoa elimu matumizi sahihi ya zebaki kwa wachimbaji

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Oryx gesi yagawa mitungi, majiko 100 kwa waandishi wa habari Dar

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gesi Tanzania imegawa mitungi 100 ya gesi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

error: Content is protected !!