Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa ACT-Wazalendo kuibana Serikali majimboni
Habari za Siasa

ACT-Wazalendo kuibana Serikali majimboni

Spread the love

 

KATIBU Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, Ado Shaibu, amesema chama chake kitaanza kuisimamia Serikali katika majimbo yote nchini, ili kuhakikisha kero za wananchi zinatatuliwa. Anaripoti Mwandishi Wetu, Ruvuma … (endelea).

Ado ametoa kauli hiyo leo Jumatano, tarehe 5 Oktoba 2022, katika ziara yake Kata ya Ligunga, wilayani Tunduru, Mkoa wa Ruvuma, baada ya baadhi ya wananchi wa wilaya hiyo kuibua changamoto sugu zinazowakabili.

“Tunduru sitowaacha. Tunafahamu kuwa madiwani na wabunge hawawajibiki kushughulikia kero zenu. Nimezunguka Tunduru Kusini na Kaskazini, kote kumejaa kero ambazo zinapaswa kufuatiliwa. Inasikitisha kuwa wabunge wa hapa wameamua kuwa mabubu Bungeni,” amesema Ado.

Miongoni mwa changamoto ambazo Ado amedai zinawakabili wananchi hao ambazo hazijafanyiwa kazi, ni uvamizi wa wanyamapori, katika makazi ya watu uliosababisha baadhi yao kupoteza maisha.

“Mimi na Mtutura (aliyekuwa Mgombea Jimbo la Tunduru Kusini), tutakuwa Wabunge wa Nje ya Bunge. Tutapaza sauti dhidi ya mauaji yanayofanywa na tembo, stakabadhi ghalani, uingizwaji holela wa Ng’ombe na kupigania huduma nzuri za kijamii kwa Wanatunduru”-alisisitiza Ndugu Ado na kuongeza:

“Utaratibu huu utakuwa kwa majimbo yote Nchini. Tutaweka utaratibu wa kuwa na sauti Nje ya Bunge ya kuwasemea wananchi. Lengo letu ni kuwa sauti mbadala ya uhakika kwa wananchi.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!