Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Rais Samia awatakia heri watahiniwa darasa la saba
Elimu

Rais Samia awatakia heri watahiniwa darasa la saba

Wanafunzi wa darasa la saba wakifanya mtihani
Spread the love

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amewatakia heri watahiniwa wanaofanya mtihani wa kuhitimu elimu ya msingi, huku akiwaahidi kwamba Serikali itahakikisha inaandaa mazingira mazuri ya kujiunga na elimu ya sekondari 2023. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Mkuu huyo wa nchi ametoa ujumbe huo leo Jumatano, tarehe 5 Oktoba 2022, ikiwa wanafunzi hao wa darasa la saba, wanaanza kufanya mitihani hiyo ya siku mbili, iliyoanza leo hadi kesho Alhamisi, tarehe 6 Oktoba mwaka huu.

“Nawatakia kila la kheri wanangu wote mnaoanza mtihani wa darasa la saba leo. Mwenyezi Mungu awape utulivu na siha njema ili mfanye vizuri mitihani yenu. Serikali itahakikisha maandalizi ya miundombinu ya kuwapokea wote watakaoendelea na kidato cha kwanza mwakani 2023 inakamilika,” ameandika Rais Samia kwenye ukurasa wake wa Twitter.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana tarehe 4 Oktoba 2022 na Kaimu Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani Tanzania (Necta), Athuman Amasi, jumla ya watahiniwa 1,384,340 wanatarajia kufanya mtihani huo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

ElimuHabari za Siasa

Walimu 52,551 kupandishwa madaraja mwaka huu

Spread the loveNaibu Waziri wa nchi, Ofisi ya Rais (Utumishi na Utawala...

BiasharaElimu

NMB yatoa vifaa vya ujenzi kwa shule sita Nyasa  

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa msaada wa vifaa mbalimbali vya ujenzi...

ElimuHabari Mchanganyiko

GGML yawapa mbinu wanafunzi Geita Boys kufikia malengo ya kitaaluma

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) imetoa mafunzo maalumu...

ElimuHabari Mchanganyiko

Wanawake GGML wawanoa wanafunzi Kalangalala Sec. kujitambua

Spread the loveKATIKA kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Wanawake Duniani, Umoja wa...

error: Content is protected !!