Thursday , 9 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Urusi yamdaka raia wa Korea Kusini kwa ushushushu
Habari MchanganyikoKimataifa

Urusi yamdaka raia wa Korea Kusini kwa ushushushu

Spread the love

Raia mmoja wa Korea Kusini amekamatwa nchini Urusi kwa madai ya ujasusi na kuzuiliwa katika mji wa mbali wa mashariki mwa nchi wa Vladivostok kabla ya kuhamishiwa Moscow kwa hatua za uchunguzi. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Shirika la habari la serikali ya Urusi – TASS jana Jumatatu limenukuu vyombo vya kisheria vikisema, mtu huyo amefahamika kwa jina la Park Won-soon.

Shirika hilo la habari la serikali limesema ni kesi ya kwanza dhidi ya raia wa Korea Kusini.

Wizara ya mambo ya nje ya Korea Kusini ilisema katika taarifa kwamba ubalozi wake mdogo ulimsaidia raia wake tangu ulipopata taarifa ya kukamatwa kwake.

Hata hivyo, ubalozi huo umejizuia kutoa maelezo zaidi kwa sababu suala hilo linaendelea kuchunguzwa.

Urusi inaichukulia Korea Kusini kama nchi isiyo rafiki kwa sababu ya uungaji mkono wa Seoul kwa vikwazo vya nchi za Magharibi dhidi ya Moscow juu ya vita vya Ukraine.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kimbunga Hidaya chaua 5, kaya 7,027 zikikosa makazi

Spread the loveSERIKALI imetoa tathmini ya athari za kimbunga Hidaya, kilichotokea tarehe...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafugaji kuku Ihemi wanufaika na mafunzo

Spread the loveWADAU  wa mnyororo wa thamani katika sekta ndogo ya kuku...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali yaainisha mpango wa kusaidia wachimbaji wadogo

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameainisha mpango wa Serikali wa...

Habari Mchanganyiko

DAWASA yatekeleza agizo la Samia kwa kutangaza zabuni kielektroniki

Spread the loveKiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Godfrey Mnzava...

error: Content is protected !!