Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Urusi yamdaka raia wa Korea Kusini kwa ushushushu
Habari MchanganyikoKimataifa

Urusi yamdaka raia wa Korea Kusini kwa ushushushu

Spread the love

Raia mmoja wa Korea Kusini amekamatwa nchini Urusi kwa madai ya ujasusi na kuzuiliwa katika mji wa mbali wa mashariki mwa nchi wa Vladivostok kabla ya kuhamishiwa Moscow kwa hatua za uchunguzi. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Shirika la habari la serikali ya Urusi – TASS jana Jumatatu limenukuu vyombo vya kisheria vikisema, mtu huyo amefahamika kwa jina la Park Won-soon.

Shirika hilo la habari la serikali limesema ni kesi ya kwanza dhidi ya raia wa Korea Kusini.

Wizara ya mambo ya nje ya Korea Kusini ilisema katika taarifa kwamba ubalozi wake mdogo ulimsaidia raia wake tangu ulipopata taarifa ya kukamatwa kwake.

Hata hivyo, ubalozi huo umejizuia kutoa maelezo zaidi kwa sababu suala hilo linaendelea kuchunguzwa.

Urusi inaichukulia Korea Kusini kama nchi isiyo rafiki kwa sababu ya uungaji mkono wa Seoul kwa vikwazo vya nchi za Magharibi dhidi ya Moscow juu ya vita vya Ukraine.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari Mchanganyiko

Polisi wakanusha kufanya uzembe ajali iliyouwa mwandishi Ayo Tv

Spread the loveJESHI la Polisi limekanusha tuhuma zilizoibuliwa dhidi yake  kwamba limekawia...

Habari Mchanganyiko

Rais Samia kuzindua gazeti litakalotoa habari za wafanyakazi Tanzania

Spread the loveSHIRIKISHO la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), liko mbioni kufufua...

Habari Mchanganyiko

GGML yaja na teknolojia za kisasa maonesho ya OSHA Arusha

Spread the loveKATIKA kuelimisha wananchi na washiriki wa maonesho ya usalama na...

error: Content is protected !!