Saturday , 11 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Chongolo ateuliwa mkuu wa mkoa Songwe
Habari za SiasaTangulizi

Chongolo ateuliwa mkuu wa mkoa Songwe

Katibu Mkuu wa CCM, Daniel Chongolo
Spread the love

Rais Samia Suluhu Hassan amemteua aliyekuwa Katibu mkuu wa CCM, Daniel Godfrey Chongolo kuwa mkuu wa mkoa wa Songwe. Chongolo amechukua nafasi ya Dk. Fransis Michael ambaye amewekwa kando. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Chongolo aliyekuwa Katibu Mkuu wa kwanza chini ya Raisi Samia Suluhu Hassan kuanzia mwaka 2021 hadi 2023 alipojiuzulu, amewahi kuhudumu kama Mkurugenzi wa Mawasiliano chini ya Idara ya Itikadi, Uenezi na Mafunzo ikiwa chini ya Nape Nnyauye.

Mwaka 2016 aliteuliwa na Rais John Magufuli kuwa Mkuu wa Wilaya ya Loliondo. Mwaka 2018 akahamishiwa Kinondoni kwa wadhifa huo huo wa ukuu wa wilaya.

Chongolo amewahi kushika nafasi zingine kama vile Mhariri wa Radio Uhuru inayomilikiwa na CCM.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Palestina mwanachama wa 194 wa UN

Spread the loveBaraza Kuu la Umoja wa Mataifa jana Ijumaa limepitisha kwa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Vijana UVCCM Kagera wataka mwenyekiti wao ajiuzulu

Spread the loveVIJANA wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Kagera wamemtaka Mwenyekiti...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina awavaa mawaziri wanaompelekea majungu Rais Samia

Spread the loveMBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina (CCM) amewataka baadhi ya mawaziri...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

THRDC, Wizara ya Katiba wajadili uanzishaji haki binadamu katika biashara

Spread the loveMTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC), umefanya...

error: Content is protected !!