Saturday , 11 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Rais mstaafu ahukumiwa miaka 4 jela
Kimataifa

Rais mstaafu ahukumiwa miaka 4 jela

Moncef Marzouki
Spread the love

Mahakama ya mjini Tunis imemhukumu rais wa zamani wa Tunisia, Moncef Marzouki kifungo cha miaka nane jela baada ya kupatikana na hatia kwa kutaka kuchochea fujo. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Marzouki, ambaye alikuwa mkuu wa kwanza wa dola kuchaguliwa kwa njia ya demokrasia baada ya vuguvugu la mapinduzi katika nchi za kiarabu mwaka 2011, anaishi nchini Ufaransa na hakuwepo mahakamani wakati hukumu hiyo ilipotolewa.

Msemaji wa mahakama amesema hukumu hiyo imetolewa kuzingatia kauli zilizotolewa na Marzouki zinazojumuisha uchochezi katika hotuba aliyoitoa mjini Paris.

Mwaka 2021 Marzouki ambaye aliiongoza Tunisia kuanzia mwaka 2011 hadi 2014, alihukumiwa kifungo cha miaka minne jela kwa kutishia usalama wa taifa baada ya kuitaka Ufaransa isitishe msaada wake kwa rais wa Tunisia Kais Saied kwenye maandamano ya mjini Paris.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Palestina mwanachama wa 194 wa UN

Spread the loveBaraza Kuu la Umoja wa Mataifa jana Ijumaa limepitisha kwa...

Habari za SiasaKimataifa

Israel yatia shubiri Gaza wakisherehekea Hamas kusitisha mapigano

Spread the loveWAKATI kundi la Hamas huko Gaza likitangaza kuridhia pendekezo lao...

KimataifaMakala & Uchambuzi

Mbivu, mbichi urais wa Ramaphosa mwezi huu

Spread the loveMWISHONI mwa mwezi huu, raia wa Afrika Kusini watapiga kura...

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

error: Content is protected !!