Monday , 13 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa 84 mbaroni kuuza sukari bei ghali
Habari za Siasa

84 mbaroni kuuza sukari bei ghali

Spread the love

Waziri wa Kilimo Hussein Bashe leo Alhamisi amesema jumla ya wafanyabiashara 84 wamekamatwa kutokana na kupandisha bei ya sukari. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Akizungumza na wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari Ikulu jijini Dar es Salaam amesema wapo katika hatua ya mwisho kupeleka mahakamani wafanyabiashara hao.

Amesema licha ya wafanyabiashara kuuziwa sukari kwa bei ya Sh 2500 hadi 2800 kwa kilo bado wameenda kuuza 4500 hadi 5000.

“Machi 15, tutakuwa tumeingiza tani 60,000 za sukari hivyo wakati wa mfungo wa Ramadhani hali itakuwa imetengamaa,” amesema Bashe.

Aidha, amesema licha ya kwamba tayari tani 31,000 zimekwisha sambazwa nchini huku tani nyingine 25,000 zikiwa zimewasili katika katika bandari ya Dar es Salaam, kwa mwaka huu Serikali itaagiza tani 300,000 za sukari kukabiliana na uhaba wa sukari nchini.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari za Siasa

Wizara afya kutumia Sh. 1.31 trilioni, huduma za kibingwa zapewa kipaumbele

Spread the loveWIZARA ya Afya, imeliomba Bunge lipitishe makadirio yake ya mapato...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Wizara kutumia Sh. 3.5 bilioni kuchunguza afya ya akili, nguvu za kiume

Spread the loveWIZARA ya Afya, imepanga kutumia Sh. 3.50 bilioni, kwa ajili...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

THRDC yapaza sauti changamoto ya intaneti

Spread the loveMTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC), umeitaka...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Prof. Ndakidemi aitaka TMA kutoa taarifa kwa njia ya SMS

Spread the loveMBUNGE wa Moshi Vijijini, Profesa Patrick Ndakidemi (CCM) ameishauri Serikali...

error: Content is protected !!