Waziri wa Kilimo Hussein Bashe leo Alhamisi amesema jumla ya wafanyabiashara 84 wamekamatwa kutokana na kupandisha bei ya sukari. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).
Akizungumza na wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari Ikulu jijini Dar es Salaam amesema wapo katika hatua ya mwisho kupeleka mahakamani wafanyabiashara hao.
Amesema licha ya wafanyabiashara kuuziwa sukari kwa bei ya Sh 2500 hadi 2800 kwa kilo bado wameenda kuuza 4500 hadi 5000.
“Machi 15, tutakuwa tumeingiza tani 60,000 za sukari hivyo wakati wa mfungo wa Ramadhani hali itakuwa imetengamaa,” amesema Bashe.
Aidha, amesema licha ya kwamba tayari tani 31,000 zimekwisha sambazwa nchini huku tani nyingine 25,000 zikiwa zimewasili katika katika bandari ya Dar es Salaam, kwa mwaka huu Serikali itaagiza tani 300,000 za sukari kukabiliana na uhaba wa sukari nchini.
Leave a comment