Tuesday , 14 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Makonda adai kuna watu wanapanga kumuua kwa sumu
Habari za Siasa

Makonda adai kuna watu wanapanga kumuua kwa sumu

Spread the love

KATIBU wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Paul Makonda, amedai kuna watu wanapanga njama za kumuuwa kwa sumu. Anaripoti Mwandishi Wetu, Songwe…(endelea).

Akizungumza katika ziara yake Tunduma, mkoani Songwe, Makonda amedai uamuzi wake wa kusema kweli bila kumung’unya maneno umewafanya baadhi ya watu kumtegemea sumu ili wamuondoe.

“Si nimepewa usemaji? nitasema kweli bila kumung’unya maneno na kwa taarifa yenu sifi na Mungu hana mpango wa kuniondoa kwanza, mtege sumu kwenye vyumba mnapoteza muda tu, mtafute waganga mnapoteza muda tu, nataka kila Kiongozi awajibike kwenye nafasi yake,”  amesema Makonda.

Msemaji huyo wa CCM amedai baadhi ya wanaopanga njama kumuuwa ni watendaji wa serikali.

“Waliopo Serikalini wote wana magari, nyumba na wanaheshimika kwa kauli ya Rais Samia Suluhu Hassan kwanini hatumsaidii kazi?, tabia ya kusubiri Rais ana ziara ndiyo mnajitokeza na mkifika pale ooh Mama unaupiga mwingi hapa ni wewe tu!, ngojeni dawa yenu inachemka,” amesema Makonda.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari za Siasa

Mbunge ataka huduma Ultrasound itolewe bure kwa wajawazito

Spread the loveMBUNGE wa Viti Maalum, Esther Malleko, ameitaka Serikali kutoa bure...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

CUF yajipanga kuelekea chaguzi zijazo

Spread the loveCHAMA cha Wananchi (CUF), kimejipanga kujijenga kisiasa kuelekea chaguzi zijazo...

Habari za SiasaKimataifa

Bunge kumuweka katibu mkuu wa EAC kikaangoni

Spread the loveAliyekuwa Katibu mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Dk. Peter...

AfyaHabari za Siasa

Wizara afya kutumia Sh. 1.31 trilioni, huduma za kibingwa zapewa kipaumbele

Spread the loveWIZARA ya Afya, imeliomba Bunge lipitishe makadirio yake ya mapato...

error: Content is protected !!