Sunday , 28 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Samia apangua, ateua wakurugenzi taasisi za umma
Habari za Siasa

Samia apangua, ateua wakurugenzi taasisi za umma

Spread the love

Rais Samia Suluhu Hassan amefanya uteuzi wa viongozi wanne katika taasisi mbalimbali ikiwa bodi ya mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Katika taarifa iliyotolewa leo Jumanne na Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Zuhura Yunus imesema Rais Samia amemtea Dk. Thomas Nestory Bwana kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI).

Dk. Bill Kiwia

Kabla ya uteuzi huu Dk. Bwana alikuwa Mkurugenzi Msaidizi Mazingira (Biodiversity Conservation) Ofisi ya Makamu wa Rais. Anachukua nafasi ya Dk. Geofrey Mkamilo ambaye amemaliza muda wake. Ameongeza kuwa uteuzi huo umeanza tarehe 3 Februari 2024.

Pia amemteua Abdul-Razag Badru kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF).

Kabla ya uteuzi huu Badru alikuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya juu (HESLB).

Aidha, aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa PSSSF, CPA Hosea Kashimba atapangiwa kazi nyingine.

Pia Rais Samia amemteua Dk. Bill Kiwia kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB).

Dk. Kiwia anachukua nafasi ya Badru ambaye ameteuliwa kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF). Uteuzi huu unaanza leo tarehe 6 Februari 2024.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Biteko aipongeza GGML kudhibiti vifo, majeruhi mahali pa kazi

Spread the loveNAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari za Siasa

Askofu Shoo awataka ACT kupigania maslahi ya Taifa, wasikubali kuhongwa

Spread the loveALIYEKUWA Askofu Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri, Askofu...

Habari za Siasa

Biteko aagiza waajiri kudhibiti vifo mahali pa kazi

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde aibana kampuni kutimiza masharti ya mkataba

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameitaka Kampuni ya Xin Tai...

error: Content is protected !!