Sunday , 28 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Makonda adai kuna watu wanapanga kumuua kwa sumu
Habari za Siasa

Makonda adai kuna watu wanapanga kumuua kwa sumu

Spread the love

KATIBU wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Paul Makonda, amedai kuna watu wanapanga njama za kumuuwa kwa sumu. Anaripoti Mwandishi Wetu, Songwe…(endelea).

Akizungumza katika ziara yake Tunduma, mkoani Songwe, Makonda amedai uamuzi wake wa kusema kweli bila kumung’unya maneno umewafanya baadhi ya watu kumtegemea sumu ili wamuondoe.

“Si nimepewa usemaji? nitasema kweli bila kumung’unya maneno na kwa taarifa yenu sifi na Mungu hana mpango wa kuniondoa kwanza, mtege sumu kwenye vyumba mnapoteza muda tu, mtafute waganga mnapoteza muda tu, nataka kila Kiongozi awajibike kwenye nafasi yake,”  amesema Makonda.

Msemaji huyo wa CCM amedai baadhi ya wanaopanga njama kumuuwa ni watendaji wa serikali.

“Waliopo Serikalini wote wana magari, nyumba na wanaheshimika kwa kauli ya Rais Samia Suluhu Hassan kwanini hatumsaidii kazi?, tabia ya kusubiri Rais ana ziara ndiyo mnajitokeza na mkifika pale ooh Mama unaupiga mwingi hapa ni wewe tu!, ngojeni dawa yenu inachemka,” amesema Makonda.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Biteko aipongeza GGML kudhibiti vifo, majeruhi mahali pa kazi

Spread the loveNAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari za Siasa

Askofu Shoo awataka ACT kupigania maslahi ya Taifa, wasikubali kuhongwa

Spread the loveALIYEKUWA Askofu Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri, Askofu...

Habari za Siasa

Biteko aagiza waajiri kudhibiti vifo mahali pa kazi

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde aibana kampuni kutimiza masharti ya mkataba

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameitaka Kampuni ya Xin Tai...

error: Content is protected !!