KATIBU wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Paul Makonda, amedai kuna watu wanapanga njama za kumuuwa kwa sumu. Anaripoti Mwandishi Wetu, Songwe…(endelea).
Akizungumza katika ziara yake Tunduma, mkoani Songwe, Makonda amedai uamuzi wake wa kusema kweli bila kumung’unya maneno umewafanya baadhi ya watu kumtegemea sumu ili wamuondoe.
“Si nimepewa usemaji? nitasema kweli bila kumung’unya maneno na kwa taarifa yenu sifi na Mungu hana mpango wa kuniondoa kwanza, mtege sumu kwenye vyumba mnapoteza muda tu, mtafute waganga mnapoteza muda tu, nataka kila Kiongozi awajibike kwenye nafasi yake,” amesema Makonda.
Msemaji huyo wa CCM amedai baadhi ya wanaopanga njama kumuuwa ni watendaji wa serikali.
“Waliopo Serikalini wote wana magari, nyumba na wanaheshimika kwa kauli ya Rais Samia Suluhu Hassan kwanini hatumsaidii kazi?, tabia ya kusubiri Rais ana ziara ndiyo mnajitokeza na mkifika pale ooh Mama unaupiga mwingi hapa ni wewe tu!, ngojeni dawa yenu inachemka,” amesema Makonda.
Leave a comment