Sunday , 12 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Tetemeko la ardhi lauwa watu 118 China
Kimataifa

Tetemeko la ardhi lauwa watu 118 China

Spread the love

TETEMEKO la ardhi lililotokea nchini China maeneo ya Kaskazini-Magharibi, limesababisha vifo vya watu zaidi ya 100 na kujeruhi 397. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa…(endelea).

Kwa mujibu wa mtandao wa BBC Swahili, tetemeko hilo limetokea usiku wa kuamkia leo Jumanne, likiwa na ukubwa wakipimo cha 5.9, lilipiga katika mikoa ya Gansu na Qinghai, nchini humo ambapo mbali ya kupoteza maisha ya watu, lilibomoa makazi.

Kufuatia tukio hilo, Rais wa China, Xi Jinping, ameagiza mamlaka za uokoaji zikatoe misaada katika maeneo yaliyoathirika.

Vyombo vya habari nchini China, vimeripoti kuwa idadi ya watu waliopoteza maisha imeongezeka hadi kufikia 118, wakati juhudi za kuwaokoa waathirika zikiendelea.

Watu takribani 20 hawajulikani na walipo, wakati 2,200 wakiokolewa huku maelfu wakikimbia makazi yao kwenda sehemu zilizo salama.

Wizara ya fedha ya China, imetenga Dola za Marekani 27.9 milioni, kwa ajili ya kushughulikia tukio hilo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Palestina mwanachama wa 194 wa UN

Spread the loveBaraza Kuu la Umoja wa Mataifa jana Ijumaa limepitisha kwa...

Habari za SiasaKimataifa

Israel yatia shubiri Gaza wakisherehekea Hamas kusitisha mapigano

Spread the loveWAKATI kundi la Hamas huko Gaza likitangaza kuridhia pendekezo lao...

KimataifaMakala & Uchambuzi

Mbivu, mbichi urais wa Ramaphosa mwezi huu

Spread the loveMWISHONI mwa mwezi huu, raia wa Afrika Kusini watapiga kura...

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

error: Content is protected !!